logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wakaazi wa Nairobi waonywa kuhusu mvua kubwa leo

Mvua ya wastani hadi kubwa inatarajiwa kulingana na ramani ya  muda wa saa 3 ya Nairobi.

image
na

Habari07 May 2024 - 12:33

Muhtasari


•Mvua ya wastani hadi kubwa inatarajiwa kuanzia alasiri, jioni na usiku kulingana na ramani ya  muda wa saa 3 ya Nairobi.

• Fahamu hali ya hewa na uwe tayari!

Wakazi wa Nairobi wameonywa kuhusu mvua  kubwa hivi leo na wametakiwa kuchukuwa tahadhari za kiusalama.

Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya imewaonya wakazi wa Nairobi kujiandaa kwa ajili ya mvua za wastani hadi kubwa zinazotarajiwa Jumanne, Mei 7, 2024.

Kulingana na idara ya hali ya hewa, mvua hiyo inatarajiwa kunyesha kuanzia alasiri hadi jioni na  usiku wa leo.

"Mvua ya wastani hadi kubwa inatarajiwa kuanzia alasiri, jioni na usiku kulingana na ramani ya  muda wa saa 3 ya Nairobi. Fahamu hali ya hewa na uwe tayari!" mtaalam wa hali ya hewa alisema katika taarifa ya   hivi karibuni.

Mnamo Jumatatu, ripoti ya hali ya hewa ilionyesha kuwa mvua itaendelea katika sehemu kubwa za nchi kwa siku saba zijazo.

Hasa, mvua kubwa inatarajiwa kunyesha katika maeneo kama vile Nyanda za Juu za Kati, Magharibi mwa Kenya, na Bonde la Ufa katika nusu ya kwanza ya kipindi hiki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved