logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua ahudhuria ibada ya kumbukumbu ya wahanga wa mafuriko ya Mai Mahiu

Gavana wa Nakuru Susan Kihika aliandamana na Gachagua.

image
na

Yanayojiri09 May 2024 - 10:18

Muhtasari


• Mbunge wa Naivasha Jane Kihara alipongeza serikali kwa hatua yake ya haraka ya kuzuia visa zaidi.

• Aliwataka wakazi kuwa waangalifu wakati huu wa mvua.

DP Gachagua ahudhuria ibada ya wafu Mai Mahiu

Naibu Rais Rigathi Gachagua amehudhuria ibada ya kuwakumbuka wahanga wa mafuriko ya Mai Mahiu.

Hafla hiyo inafanyika katika Viwanja vya Mo Gas huko Mai Mahiu, Nakuru.

Gavana wa Nakuru Susan Kihika aliandamana na Gachagua.

Viongozi wengine ni Ann Wamuratha (Kiambu), Martha Wangari (Gilgil), Mburu Kahangara (Lari), George Koimburi (Juja) na Simon King'ara (Ruiru).

Wengine ni pamoja na Kamande Mwafrika (Roysambu), Jane Kihara (Naivasha), na Mary Wa Maua (Maragua) miongoni mwa wengine.

Mkasa wa Mai Mahiu ulisababisha vifo vya watu 60, huku watu 51 wakiwa bado hawajulikani waliko na wengine 52 kupata majeraha wakati wa matukio yaliyotokea wiki iliyopita.

Mbunge wa Naivasha Jane Kihara alipongeza serikali kwa hatua yake ya haraka ya kuzuia visa zaidi.

Aliwataka wakazi kuwa waangalifu wakati huu wa mvua.

"Tuna furaha kuwa na naibu rais hapa kutufariji na tuna furaha," Kihara alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved