NTSA yatoa hatua za kuzingatiwa wakati shule zinapofunguliwa tena

"Pamoja tuhakikishe watoto wetu wamefika shuleni salama," NTSA ilisema.

Muhtasari

•  Magari hayo pia yanatakiwa kuwa na cheti halali cha ukaguzi na Leseni halali ya Huduma ya Barabara (RSL).

• Magari yote ya usafiri wa shule lazima yawe na mikanda ya usalama na bima halali ya magari.

Basi la shule.
Basi la shule.
Image: NTSA//X

Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama  barabarani (NTSA) imetaja hatua kali kwa shule huku kukiwa na ukaguzi unaoendelea wa kufuata usalama barabarani kote nchini.

Katika hatua iliyokusudiwa kuimarisha usalama barabarani kwa wanafunzi wanaporejea shuleni, mamlaka ya uchukuzi ilitangaza kwamba ni lazima magari yote ya usafiri wa shule yawe na kidhibiti mwendo kinachofanya kazi kwenye Mfumo wa Usalama Barabarani wa NTSA (RSMS).

"Taasisi/magari ya uchukuzi wa shule yanayofanyiwa ukaguzi wa kufuata sheria za usalama barabarani katika maeneo mbalimbali nchini," taarifa ya NTSA inasomeka katika sehemu.

Magari hayo pia yanatakiwa kuwa na cheti halali cha ukaguzi na Leseni halali ya Huduma ya Barabara (RSL).

Vile vile, NTSA ilionya dhidi ya kupakia kupita kiasi na kusema kuwa magari yote ya usafiri wa shule lazima yawe na mikanda ya usalama na bima halali ya magari.

Wakala wa barabara pia walibainisha kuwa dereva lazima awe na uthibitisho unaohitajika wa cheti cha kuendesha  gari na beji halali ya PSV inayosisitiza kwamba wasimamizi wote wa shule lazima waweke hatua ili kuhakikisha utiifu kamili wa mahitaji ya Sheria ya Trafiki na kanuni za PSV.

Zaidi ya hayo, NTSA ilitoa wito kwa madereva wa magari kuwa waangalifu barabarani na kuzingatia watumiaji wengine wa barabara na watoto wanaoripoti shuleni.

"Usimamizi wa shule LAZIMA uweke hatua za kuhakikisha Ufuasi kamili wa matakwa ya Sheria ya Trafiki na kanuni za PSV. Tunawataka madereva wote wa magari kuwa waangalifu na kuwa makini na watumiaji wengine wa barabara watoto wanaporejea shuleni," NTSA iliongeza.

"Pamoja tuhakikishe watoto wetu wamefika shuleni salama," NTSA ilisema