"Tutarudi kwenye maandamano!"- Kalonzo anaonya kuhusu Mswada wa Fedha wa 2024

Kama muungano, tuko tayari kurejea kwenye maandamano ikiwa ni hivyo. Natumai una ujasiri wa kutosha. Muwe tayari mabibi na mabwana.

Muhtasari

• Kama muungano, tuko tayari kurejea kwenye maandamano ikiwa ni hivyo. Natumai una ujasiri wa kutosha. Muwe tayari mabibi na mabwana.

KALONZO MUSYOKA
Image: HISANI

Kalonzo Musyoka ametishia kuandaa maandamano kote nchini kuhusu mapendekezo ya Mswada wa Fedha wa 2024.

Alikuwa akizungumza  siku ya Jumatano  baada ya mkutano wa kundi la wabunge wa Azimio.

Musyoka alimwambia Rais William Ruto kwamba Wakenya hawataketi huku wabunge wakiidhinisha Mswada huo wa ‘dhalilishiadhabu’.

 

"Kama muungano, tuko tayari kurejea kwenye maandamano ikiwa ni hivyo. Natumai una ujasiri wa kutosha. Muwe tayari mabibi na mabwana.

"Ikiwa unahisi dhaifu kiasi kwamba unafikiri huwezi kuhimili duru nyingine ya maandamano, basi nenda kula kitu chenye nguvu kwa sababu tunakuhitaji na nchi hii inakuhitaji," alisisitiza.

Juu ya ajenda zao katika mkutano huo ilikuwa Mswada wa Sheria ya Fedha 2024 na ripoti ya Kamati ya Kitaifa ya Majadiliano.

Mswada wa Sheria ya Fedha wa 2024, ambao ulichapishwa Mei 9, unatarajiwa kushirikishwa na umma kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Kitaifa kwa mjadala.

Maseneta na wabunge kutoka Azimio leo walifahamishwa na baraza la uchumi la muungano huo kuhusu vipengele vyenye utata vya Mswada huo.

Katibu Mkuu wa  (ODM) Edwin Sifuna alisema warsha hiyo ni muhimu kuwapa uwezo wabunge kuunda upinzani mkali dhidi mswada huo wakati wa mjadala.

Ushuru wa magari unaopendekezwa wa asilimia 2.5 tayari unaibua hisia tofauti kutoka kwa Wakenya na mgawanyiko wa kisiasa.

Kulingana na Mswada huo, kila gari litalipa angalau KSh5,000 ushuru wa mwaka na kiwango cha juu cha KSh100,000.

Wakenya pia watalipa zaidi kwa miamala ya pesa kwa simu huku serikali ikipanga kuongeza ushuru kwa kampuni za mawasiliano kama vile M-Pesa na benki ya simu.