9 wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya matatu kutumbukia mto Mbagathi

Walisema kuwa watu wengine waliokuwa ndani ya gari hilo ambao walipata majeraha walikimbizwa katika hospitali za karibu kwa matibabu.

Muhtasari

• Polisi walitahadharisha kuwa kuna msongamano mkubwa wa magari barabarani na kuwataka madereva kutumia njia mbadala.

Image: HISANI

Takriban watu wanane wamepoteza maisha baada ya matatu kutumbukia mto Mbagathi Jumamosi asubuhi.

Kulingana na ripoti ya polisi iliyoonwa na gazeti la Star, tukio hilo lilitokea saa 10 alfajiri, likihusisha matatu ya kubeba watu 33.

Wanane hao walikufa papo hapo.

Polisi walisema matatu hiyo ilipoteza udhibiti kabla ya kutumbukia mtoni.

"Leo asubuhi 18/05/24 mwendo wa 10:00 asubuhi matatu ya PSV iliyokuwa ikipitia njia ya Gataka Nairobi ilipoteza mwelekeo na kutumbukia kwenye mto Mbagathi kabla tu ya Chuo Kikuu cha Cooperative kuwaua watu 8 papo hapo," ripoti ya Polisi ilisema.

Walisema kuwa watu wengine waliokuwa ndani ya gari hilo ambao walipata majeraha walikimbizwa katika hospitali za karibu kwa matibabu.

"Wengine waliokolewa na magari mbalimbali ya kubebea wagonjwa na kupelekwa katika hospitali za karibu ingawa walikuwa katika hali mbaya."

Polisi walitahadharisha kuwa kuna msongamano mkubwa wa magari barabarani na kuwataka madereva kutumia njia mbadala.

Ajali hiyo inajiri huku Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama (NTSA) ikiimarisha kampeni zake za kuhamasishwa kuhusu usalama barabarani, kote nchini.

Kulingana na NTSA, vifo 1,553 vilitokea kutokana na ajali za barabarani kuanzia Januari 1 hadi Aprili 30, 2024.

Nairobi ilirekodi idadi kubwa zaidi ya walioaga wakiwa 176, ikifuatwa na Nakuru na Kiambu katika 134 na 128 mtawalia.

Kisumu ilirekodi vifo 59, Machakos 56, Kilifi, Meru, Murang'a na Uasin Gishu ilirekodi visa 50 kila moja, na Narok vifo 48.

Bungoma ilikuwa na vifo 44, Kaka mega na Makueni 41 kila moja, Kisii 38, Nyeri 37, Kajiado 34, Kirinyaga 33 na Bomet 31.

Kitui na Migori wana vifo 30 vilivyorekodiwa kila mmoja, Taita Taveta na Trans Nzoia 28 kila mmoja, Kericho 27, Embu na Siaya 24 kila mmoja, na Tharaka Nithi ana 22.

Laikipia na Turkana kila moja ilikuwa na vifo 21, Vihiga 20, Busia, Mombasa na Nyandarua 19 kila moja, Baringo na Homa Bay 18, Nyamira 17, Kwale 15, na Nandi 13.

Elgeyo Marakwet ilikuwa na visa 8, Garissa 7, Pokot Magharibi 6, Wajir 5, Tana River 4, Isiolo 3, kwani Lamu, Mandera, Samburu walikuwa na vifo viwili kila moja.