DP Gachagua aahidi ufadhili kamili wa masomo kwa mshairi wa umri wa Miaka 11

Princess Angel pia atajiunga na Chuo cha Utawala jijini Nairobi, ambapo atapata fursa ya kuunda na kuimarisha ujuzi wake.

Muhtasari
  • Katika taarifa fupi kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, kamanda wa pili alimpongeza Princess Angel kwa umahiri wake wa kutunga mashairi katika lugha ya Kiingereza na Kiswahili.
NAIBU RAIS RIGATHI GACHAGUA NA MSHAHIRI PRINCESS ANGEL
Image: DP GACHAGUA/ X

Princess Angel mwenye umri wa miaka 11 anaweza kuwa katika njia ya kufikia ndoto yake ya kuwa wakili baada ya Naibu Rais Rigathi Gachagua kujitolea kufadhili elimu yake.

Katika taarifa fupi kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, kamanda wa pili alimpongeza Princess Angel kwa umahiri wake wa kutunga mashairi katika lugha ya Kiingereza na Kiswahili.

Kulingana na Gachagua, aliguswa moyo na umilisi mkubwa wa msichana huyo wa lugha hizo mbili na ustadi wa kustarehesha wa uimbaji wakati wa Kongamano la Maombi la Kitaifa la Akurinu huko Nakuru.

Kielelezo cha msichana huyo cha ustadi wa lugha kilichochea Naibu Rais na Mama wa Pili, Dorcas Rigathi kumwalika Angel katika makazi ya Gachagua huko Karen, Nairobi.

"Nilifurahiya asubuhi ya leo, pamoja na Mwenzi wangu Mchungaji Dorcas Rigathi, kuwakaribisha Binti mrembo na mamake Ann Kariuki kwa kiamsha kinywa katika Makao Rasmi ya Karen, Nairobi," Naibu Rais alisema.

"Tumetambua talanta; tunataka kumkuza hadi kufikia uwezo kamili," Gachagua aliongeza.

Kufuatia mwaliko huo, DP Gachagua na kasisi Dorcas waliahidi Princess Angel ufadhili wa elimu kamili hadi ngazi yake ya elimu ya juu.

Princess Angel pia atajiunga na Chuo cha Utawala jijini Nairobi, ambapo atapata fursa ya kuunda na kuimarisha ujuzi wake.

"Nitashughulikia mahitaji yake ya elimu hadi awe Mwanasheria mzito anayetamani kuwa," Gachagua alisema.

Gachagua alitoa ahadi hiyo alipozuru chuo kikuu ambapo alifanya mazungumzo na wanafunzi. "Nitalipa karo ya shule kwa wanafunzi 10 ambao ni wahitaji sana kama kumbukumbu ya ziara yangu," alisema Naibu Rais.