logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majeneza kadhaa yatapakazwa katikati mwa jiji la Nairobi na waandamanaji (video)

Majeneza hayo zaidi ya 10 ya rangi ya kahawia hayajulikani yalikotolewa.

image
na Davis Ojiambo

Habari02 July 2024 - 12:02

Muhtasari


  • •   Tukio hili liliwaacha polisi kwa mshangao wasijue cha kufanya kwa mara moja kabla ya kuanza kuyainua na kuyaweka ndani ya lori moja la rangi nyeupe.
Majeneza ya maandamano

Kisa kisicho cha kawaida kimeshuhudiwa mchana wa Jumanne katikati mwa jiji la Nairobi wakati waandamanaji waliamua kutapakaza majeneza Zaidi ya 10 kwenye barabara wakati wa maandamano yao.

Maandamano hayo ambayo yanaelekezwa dhidi ya serikali na haswa uongozi wa rais William Ruto, wengine wakishinikiza kung’atuka kwake madarakani kama rais.

Cha kushangaza ni kwamba wakati polisi wanhaha juu na chini kuwatuliza waandamanaji kwa kuwasambaratisha kwa kutumia vitoza machozi, wengine walitokea kusikojulikana wakiwa wamebeba majeneza na kuyaweka katikati ya barabara.

Tukio hili liliwaacha polisi kwa mshangao wasijue cha kufanya kwa mara moja kabla ya kuanza kuyainua na kuyaweka ndani ya lori moja la rangi nyeupe.

Baadhi ya waandamanaji walionekana wakitokea katika barabara mbalimbali karibu na bustani ya Jevanjee wakiwa na majeneza hayo kabla ya kuyatelekeza katikati mwa barabara ya Moi Avenue.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved