Mshukiwa mkuu wa mauaji ya wanawake katika eneo la Kware akamatwa

Kulingana na polisi, mshukiwa amekiri mauaji hayo ya mfululizo.

Muhtasari

•Mshukiwa alikamatwa siku ya Jumatatu asubuhi katika eneo la Kayole alikokuwa amejificha, maafisa walisema.

•Hata hivyo anakaa takriban mita 500 kutoka eneo la taka la Kware ambapo takriban miili kumi ya wanawake iliyoharibika vibaya imepatikana katika operesheni.

Miili hiyo ilitolewa kwenye eneo la taka Kware, kaunti ya Nairobi mnamo Julai 12, 2024
Image: Star

Polisi walitangaza  mnamo Jumatatu kuwa walikuwa wamefanya uchunguzi kuhusu mauaji ya baadhi ya watu ambao miili yao ilikuwa imetolewa kutoka eneo la kutupa taka katika eneo la Kware, mtaa wa mabanda wa Mukuru, Nairobi.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai Mohamed Amin  mnamo Jumatatu Julai 15 asubuhi ameratibiwa kufanya mkutano na waandishi wa habari kuhusu matukio ya hivi punde katika matukio hayo.

Mshukiwa alikamatwa siku ya Jumatatu asubuhi katika eneo la Kayole alikokuwa amejificha, maafisa walisema.

Inaripotiwa kwamba anakaa takriban mita 500 kutoka eneo la taka la Kware ambapo takriban miili kumi ya wanawake iliyoharibiwa vibaya imepatikana katika operesheni.

Kulingana na polisi, mshukiwa alikiri mauaji hayo ya mfululizo.

Afisa mmoja alimtaja kama punguani.

Alifukuzwa hadi kwenye nyumba moja mtaa wa Kayole ambapo maafisa walisema alikuwa akijaribu tena kumrubuni mwathiriwa.

Vyanzo vya habari vilisema uvamizi wa nyumba ya mshukiwa ulisababisha kupatikana kwa simu kumi, vitambulisho saba, sim kadi kumi, panga, glovu, na magunia kadhaa sawa na yale yaliyokutwa na miili kwenye eneo la taka na kamba.

"Tunaamini tuna mshukiwa mkuu na mkuu wa mauaji ya watu ambao miili yao imepatikana imetupwa katika eneo la Kware," alisema afisa mmoja anayefahamu suala hilo.

Maafisa wa upelelezi kutoka makao makuu ya DCI katika operesheni hiyo pia walifuatilia pesa zilizotolewa kutoka kwa waathiriwa wa hivi punde wa mauaji hayo.

Polisi walitaja matukio hayo kuwa mafanikio katika uchunguzi ambao ulitishia serikali huku kukiwa na madai ya mauaji ya kiholela.

Simu ya rununu ya mmoja wa waathiriwa aliyetambuliwa kufikia sasa -Josephine Owino- ilipatikana kutoka kwa mshukiwa aliyekuwa kizuizini.

Hadi sasa wanawake wawili akiwemo Josephine wametambuliwa.

Josephine alitoweka mnamo Juni 26 huku mwathirika wa pili alitoweka mnamo Juni 28.

Dadake Josephine alisema alipokea simu kutoka kwa mwanamume ambaye alimwambia alikuwa na mwathiriwa.

Hakurudi nyumbani. Mwili wake ulipatikana ukiwa umeingizwa kwenye gunia kwenye eneo la kutupia taka.

Mchakato wa kuwatambua wahasiriwa wengine unaendelea.