Tunataka majibu! Rais wa LSK baada ya polisi kuwarushia watoto vitoa machozi Kakamega

Katika video inayosambaa mitandaoni watoto hao wanaonekana wakipambana na makali ya vitoa machozi.

Muhtasari
  • Hiii ni baada ya maandamano ya kupinga serikali ya Gen Z kuendelea Jumanne katika maeneo tofauti na kaunti tofauti Nchini.
Image: SCREENGRAB

Rais wa Chama cha Wanasheria nchini Kenya, Faith Odhiambo amelaani vikali kitendo cha polisi kuwarushia watoto waliokuwa shule vitoa machozi Kakamega.

Katika video inayosambaa mitandaoni watoto hao wanaonekana wakipambana na makali ya vitoa machozi.

Hiii ni baada ya maandamano ya kupinga serikali ya Gen Z kuendelea Jumanne katika maeneo tofauti na kaunti tofauti Nchini.

Rais huyo wa LSK amesema kwamba watoto hawapaswi kushambuliwa.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa X Rais Huyo wa LSK alilaani vikali kitendo cha polisi kuwarushia watoto mabomu ya vitoa machozi.

"Watoto hawapaswi kushambuliwa kamwe, tunahitaji majibu," Faith alisema.

Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Idara ya Huduma kwa Polisi imetoa taarifa ya tahadhari kabla ya maandamano yaliyopangwa kufanyika leo, Julai 16.

Vijana wa Kenya wamekuwa wakiongoza maandamano dhidi ya serikali na sera zake katika wiki chache zilizopita na shughuli zaidi zinatarajiwa Jumanne.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa Jumanne asubuhi, Kaimu Inspekta Jenerali wa polisi, Douglas Kanja Kirocho alibainisha kuwa baadhi ya makundi ya wahalifu yanapanga kujipenyeza na kuvuruga maandamano hayo ya amani, hatua ambayo inaweza kuvuruga amani na usalama wa waandamanaji.

"Hata hivyo, katika kipindi cha hivi majuzi, tumeshuhudia kwa masikitiko makubwa vifo vya watu, majeraha, vurugu, uhalifu na uharibifu wa mali kutokana na maandamano ya aina hiyo, na kusababisha uchungu na mateso kwa familia na kuvurugika kwa biashara na shughuli za kawaida za kufanya kazi. maelfu ya Wakenya.

Asubuhi ya leo, tulipokea taarifa za kijasusi za kuaminika zinazoonyesha kwamba makundi fulani ya wahalifu waliopangwa wamepanga kujipenyeza, kuvuruga na kutatiza hali ya amani ya maandamano hayo, jambo ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa waandamanaji,” IG Kanja alisema.