logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama maeneo yatakayoathirika na kukatizwa kwa umeme Jumapili- KPLC

Baadhi ya maeneo ya kaunti mbili za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 May 2024 - 06:13

Muhtasari


•KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumapili, Mei 5.

•Baadhi ya maeneo ya kaunti mbili za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumapili, Mei 5.

Katika taarifa ya Jumamosi jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti mbili za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.Kaunti ambazo zitaathirika ni Uasin Gishu na Homa Bay.

"Habari za jioni. Maeneo yaliyoorodheshwa yataathiriwa na kukatizwa kwa umeme kesho Jumamosi (5 Mei, 2024). Kukatizwa ni sehemu ya matengenezo ya mtandao. Kwa ilani ya mapema, tumia http://bit.ly/31u4jY4. Ili kufikia ratiba ya hivi punde, angalia chini ya tarehe ya hivi majuzi zaidi," KPLC ilisema katika taarifa ya Jumamosi,

Katika kaunti ya Uasin Gishu, maeneo kadhaa yakiwemo CBD, Eagle, Sugar Land Plaza na viunga vyao yatakosa umeme kati ya saa nne asubuhi na saa tisa alasiri.

Katika kaunti ya Homa Bay, baadhi ya maeneo yakiwemo Nyabola, Mwamba, Jerusalem na viunga vyao yataathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved