logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Niliwapata mchana peupe-Mwanamke asimulia jinsi mama yake alivyomnyakua mpenzi wake

Hiyo ni laana, natamani ningemjua baba yangu mzazi."

image
na Radio Jambo

Habari21 April 2022 - 13:43

Muhtasari


  • Mwanamke asimulia jinsi mama yake alivyomnyakua mpenzi wake

sad woman

Tumekuwa tukiyaona kwenye filamu, na kupuuzilia mbali huku tukisema kwamba ni uigizaji tu na hamna mtu ambaye ana akili timamu anawea fanya mambo mengine.

Hata wazazi wakati huu na karne hii hawaheshimu ndoa za watoto wao, kwani wameona tu ni jambo la kawaida kuishi na watoto wao baada ya kufunga harusi.

Mwandadammoja aliwaacha wanamitandao midomo wazi baada ya kufichua kwamba mama yake alimnyakulia mpenzi wake miezi chache tu baada ya kufunga pingu za maisha na mpenziwe.

Huu hapa usimulizi wake;

"Kusema ukweli sijawahi ona kwamba nina mama, ndio amenilea na sijawahi jua baba yangu mzazi,ni jambo ambalo hakutaka kuniambia au tulizungumzie tukiwa sebuleni

Niliweza kufunga ndoa nikiwa na miaka 28, lakini sikujua kwamba mama yangu alikuwa tayari kwenye uhusiano na mume wangu

Siku moja niliwapata mchana peupe wakiwa kwenye mahaba tele, nilienda kazi na kurudi bila kuwataarifu, hapo ndipo nilikata uhusiano wangu na mama yangu na mume wangu, na sioni kama nitawahi msamehe mama yangu, kwa kumkubali mwanamume aliyekuwa na uhusiano naye kunioa

Hiyo ni laana, natamani ningemjua baba yangu mzazi."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved