logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makamishna waliojitenga ndio walienda Ugiriki kuangalia uchapishaji - wakili Kamau Karori

“Kabla ya karatasi za kupiga kura zisafirishwe nchini, makamishna ambao sasa ni walalamishi walikwenda nchini Ugiriki kufanya uangalizi jinsi uchapishaji " - Kamau Karori

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 September 2022 - 08:43

Muhtasari


• Alitilia shaka kujitenga kwa mawakili wanne licha ya kwamab wao ndio waliwakilisha tume huko Ugiriki katika shughuli ya kuangalia uchapishaji wa karatasi za kupiga kura.

Mwanasheria Kamau Karori akiwakilisha IEBC

Wakili wa mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC mwanasheria Kamau Karori amemtetea vikali Chebukati dhidi ya shtuma zilizotolewa na makamishne wanne waliojitenga na matokeo ya uchaguzi wa urais.

Katika utetezi wake, Karori alisema kauli ambayo ilionekana kuwiana na swali la jaji Lenaola aliyetilia shaka kujiondoa kwa makamishna hao kwa madai kwamab hawawezi kujihusisha na matokeo hayo licha ya kuonekana awali kuyatangaza huku shughuli ya kuhesabu kura ilipokuwa ikiendelea.

Karori alisema kwamba makamishna hao wanne waliojitenga na matokeo walisafiri mpaka nchini Ugiriki kukagua karatasi na vifaa vyote vya kuendesha shughuli ya uchaguzi.

Makamishna hao ndio waliwakilisha tume ya IEBC katika uangalizi wa shughuli ya uchapishaji wa karatasi za kupiga kura kulingana na Karori.

Kulingana na wasilisho la Karori katika kutetea tume ya IEBC na Mwenyekiti wake, makamishna wanne waasi hawana sababu yoyote ya kujitenga na uchaguzi pamoja na matokeo yote kwani walionekana hadharani wakishiriki katika mchakato wote usiku na mchana.

“Kabla ya karatasi za kupiga kura zisafirishwe nchini, makamishna ambao sasa ni walalamishi walikwenda nchini Ugiriki kufanya uangalizi jinsi uchapishaji ulivyokuwa ukiendelea. Wao ndio waliwakilisha tume ya IEBC huko,” Karori alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved