logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Marais wa Afrika walisafiria gari la kubeba maiti kuenda kuona maiti - Babu Owino

Unaondokaje Kenya na matatizo yake yote kwenda kuona maiti London bado unadai kwamba hakuna pesa Kenya - Babu Owino.

image
na Radio Jambo

Burudani19 September 2022 - 11:40

Muhtasari


• Marais wa Afrika walibebwa kwenye gari la kubebea maiti kwenda kumwona marehemu Malkia - Babu Owino.

Babu Owino akejeli hatua ya marais wa Afrika kusafiri Uingereza kwa mazishi ya malkia Elizabeth 2

Mbunge wa Embakasi East Babu Owino amekuwa mtu wa hivi punde kuzungumzia suala la marais wa Afrika kusafirishwa kwa basi kuelekea eneo la hafla ya msiba wa malkia wa Uingereza, Elizabeth II.

Babu Owino katika ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, amemtupia kiazi moto kinywani rais William Ruto kwa kile alisema kwamba kuondoka Afrika ili kuelekea ughaibuni kuona maiti ni hulka ya kizamani.

Babu Owino alionekana kufurahia kitendo hicho amabcho marais wa Afrika walifanyiwa kusafirishwa kwa mkupuo katika basi moja.

Kulingana na mbunge huyo mkosoaji mkubwa wa serikali ya Ruto, haina haja mtu kusafiri kuenda Uingereza kuona maiti kwa sababu kuna kazi nyingi za muhimu huku nyumbani ambazo mtu anaweza akafanya.

Owino alimsuta Ruto na uongozi wake kwa kudai kwamba uongozi ulioondoka ulifyonza kila kitu kutoka kwa akaunti za serikali. Alisema kwamba kauli hizo ni uongo kwani haiwezekani waseme hakuna pesa kwenye akaunti ilhali wanaendelea kutumia hizo pesa kufanya ziara kote duniani.

“Marais wa Afrika walibebwa kwenye gari la kubebea maiti kwenda kumwona marehemu Malkia. Unaondokaje Kenya na matatizo yake yote kwenda kuona maiti London bado unadai kwamba hakuna pesa Kenya!!!Hustlers mtajionea mambo,” Owino aliandika.

Rais Kenyatta aliondoka wikendi iliyoita kuelekea Uingereza kushiriki hafla ya mazishi ya malkia Elizabeth wa pili akiongozana na mama Rachael Ruto.

Baadae ataondoka kuelekea Marekani kwa hafla ya 77 ya kongamano la umoja wa mataifa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved