logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Toto asherehekea siku ya mashujaa akikata mboga kijijini

Ninakumbuka vijana wa Kenya ambao wanatoka katika malezi duni lakini wanajitahidi sana na kujitolea sana kubadilisha maisha - Toto.

image
na Radio Jambo

Habari20 October 2022 - 11:43

Muhtasari


• Toto aligonga vichwa vya habari baada ya kushinda uwakilishi wanawake kaunti ya Bomet akiwa na umri mchanga.

Toto asherehekea mashujaa akikata mboga kijijini

Mwakilishi wa Wanawake katika kaunti ya Bomet Linet Chepkorir almaarufu Toto amewasherehekea Wakenya wapambanaji wa kipato cha kadri almaarufu mahasla kwa ujumbe maalum kama mashujaa wake.

Toto ambaye aliingia kweney vitabu vya historia kuwa mwanamke mchanga zaidi kuwahi kushinda wadhifa huo na kuwa miongoni mwa wanasiasa wachanga katika bunge la kitaifa alisema kwamba wananchi hao wanaopambana mchana na usiku kutafuta riziki wanafaa kuheshimiwa na kupewa sifa kwani bila wao uchumi wa nchi hautakua kwa njia yoyote.

Alipakia picha yake akiwa kijijini mwao huku akikata kabichi, kama kujikumbusha maisha ambayo alikuwa anapitia kabla ya kupanda ngazi katika uongozi wa kaunti ya Bomet.

“Tunapoadhimisha mashujaa mashuhuri, pia ninakumbuka vijana wa Kenya ambao wanatoka katika malezi duni lakini wanajitahidi sana na kujitolea sana kubadilisha maisha yao na taswira ya nyumba zao. Ninyi pia ni mashujaa. Heri ya Siku ya Mashujaa!” Toto aliandika kwenye picha hiyo.

Alhamisi, rais William Ruto aliongoza sherehe za mashujaa katika uwanja wa Uhuru Gardens ambapo hotuba yake ya zaidi ya dakika 20 ilijawa wingi wa mipango yake katika kuboresha uchumi wa taifa la Kenya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved