logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa kuwa waziri mkuu wa Pakistan Imran adai haki kwa mwanahabari Arshad Sharif

Habari za kifo cha Sharif zilileta mshtuko kote ulimwenguni baada ya kuripotiwa kuuawa

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 October 2022 - 12:46

Muhtasari


  • Habari za kifo cha Sharif zilileta mshtuko kote ulimwenguni baada ya kuripotiwa kuuawa na maafisa wa polisi Jumapili usiku
Mwanahabari Arshad Sharif

Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistani Imran Khan ameungana na Wapakistani na waombolezaji kote ulimwenguni kutaka wale waliohusika na kifo cha mwanahabari maarufu Arshad Sharif waadhibiwe.

Khan kupitia kwenye ukurasa wake wa Twitter Jumatatu, huku kukiwa na rundo la jumbe za rambirambi, aliomboleza Sharif kama mwanahabari mahiri na shupavu ambaye hakuwahi kuogopa kusema ukweli.

"Nilishangazwa na mauaji ya kikatili ya Arshad Sharif ambaye alilipa gharama kubwa kwa kusema ukweli - maisha yake. Ilibidi aondoke nchini na kujificha nje ya nchi lakini aliendelea kusema ukweli kwenye mitandao ya kijamii, akiwafichua wenye nguvu. Taifa zima linaomboleza kifo chake," aliandika kwenye.

Alitoa wito wa uchunguzi mkali ufanyike kuhusu mauaji hayo na kuwafikisha wahusika mahakamani.

"Uchunguzi sahihi wa kimahakama lazima uanzishwe ili kuchunguza kauli zake mwenyewe pamoja na ushahidi ambao vyanzo vingine vinao. Tumeingia katika hali ya ukatili, isiyojulikana katika jamii iliyostaarabika, iliyoingizwa na wenye nguvu dhidi ya wale wanaothubutu kukosoa na kufichua maovu," alibainisha.

Habari za kifo cha Sharif zilileta mshtuko kote ulimwenguni baada ya kuripotiwa kuuawa na maafisa wa polisi Jumapili usiku.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved