logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Unampotosha Raila,'Didmus Barasa amwambia Makau Mutua

Hii ni baada ya Mutua siku ya Jumamosi kusema kwamba  uchaguzi wa urais nchini haujaisha.

image
na Radio Jambo

Makala06 November 2022 - 08:02

Muhtasari


  • Mwezi uliopita, Karua alidokeza kupeleka suala hilo katika Mahakama ya Afrika Mashariki

Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa kupitia ukrasa wake wa twitter, amemrushia vijembe msemaji wa Azimio Makau Mutua.

Hii ni baada ya Mutua siku ya Jumamosi kusema kwamba  uchaguzi wa urais nchini haujaisha.

"Hakuna anayepaswa kufikiria kuwa uchaguzi wa urais wa Kenya umekwisha. Hatujawahi kukubali chochote. Kaa chonjo," Mutua alisema.

Barasa alimwambia Mutua kwamba anampotosha Raila, na anapaswa kumuacha Raila ataafu polepole.

"Hawa watu wanaompa ushauri @RailaOdinga ndio wanampa shinikizo badala ya kumwacha Aende Retire polepole.Kenya tayari ishaa endelea rafiki zangu @makaumutua unampotosha g Raila,"Barasa Alisema.

Kauli hiyo inajiri  baada ya kiongozi wa chama cha Narc Kenya Martha Karua kuwasilisha ombi katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki kupinga uamuzi wa Mahakama ya upeo kuhusu uchaguzi wa urais wa 2022.

Katika marejeleo yaliyowasilishwa kortini Ijumaa, Karua na Mwanaharakati Khelif Khalifa wanateta kuwa IEBC na Mahakama ya Juu zilipuuza demokrasia na kuhujumu utawala wa sheria kupitia hatua zao katika uchaguzi wa urais wa 2022.

Mwezi uliopita, Karua alidokeza kupeleka suala hilo katika Mahakama ya Afrika Mashariki.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved