logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Natembeya aahidi kumtuza muuguzi aliyewatumbuiza watoto wagonjwa

George Natembeya aliahidi kumlipia Elizabeth Robai karo kwa kuwa na bidii

image
na Radio Jambo

Habari09 November 2022 - 05:29

Muhtasari


• Gavana Natembeya alikuwa amevutiwa na video ya Elizabeth akiwachezea watoto wimbo maarufu wa kuwatuliza watoto wa 'Baby Shark' .

• Video ya Elizabeth akiwachezea watoto ilisambaa na kuibua hisia tofauti.

Gavana wa kaunti ya Trans Nzoia George Natembeya, ameahidi kumtuza binti ambaye aligeuka gumzo mtandaoni baada ya klipu yake akiwachezea watoto kusambaa.

Binti huyo ambaye ni mwanfunzi wa Kenya Medial Training College( KMTC) alikuwa anawachezea watoto katika wodi ya hospitali ya Kitale.

Natembeya alikuwa amefurahishwa na jambo la Elizabeth Robai kwa tendo lake la wema la kuwachezea watoto hospitalini.

Alimwalika Elizabeth Robai katika ofisi yake ili kumpongeza kwa kazi yake kisha kumpa hakikisho la kumtuza.

"Jioni hii nilimwalika muuguzi wa watoto Elizabeth Robai Lukelesia, mwanafunzi katika Chuo cha mafunzo ya matibabu (KMTC) ambaye alivuma baada ya video yake kusambaa akimtumbuiza mtoto katika hospitali ya Kitale level IV," Natembeya aliandika.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Natembeya alizidi kufafanua jinsi atakavyomtuza mrembo huyo.

"Nimeahidi kulipia masomo yake kwa wakati mdogo uliobaki ili kumaliza masomo yake. Nitahakikisha kuwa ataajiriwa kama mwanafunzi ili kupata mafunzo kisha kutambulika na kuweza kuhudumu kama mwuguzi wa watoto. Hongera Elizabeth Robai, bidii na kujitolea kwako imezaa matunda," Gavana huyo alisema.

Kabla ya kukutana na binti huyo, Gavana Natembeya alikuwa ametangaza jinsi alivyokuwa amevutiwa na jambo hilo.

"Nimevutiwa na matukio ya kusisimua ya muuguzi wa watoto, Elizabeth Robai Lukelesia akimtumbuiza mtoto anayepona.Kazi nzuri Elizabeth, uwajibikaji katika utoaji wa huduma ndiyo kauli mbiu yetu kuu," George Natembeya aliandika.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved