logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mnaopinga sera yetu ya GMO mtaungua jehanamu!" - Kuria amjibu Raila na timu yake

Mnandelea kushambulia sera yetu ya GMO huku Hustlers wakifa kwa njaa na nyama ya punda yenye sumu. Mtaungua kuzimu - Kuria

image
na Radio Jambo

Habari20 November 2022 - 10:53

Muhtasari


• Kulingana na bwana Raila, suala la GMO si jambo la kukurupukiwa tu hivi bali linahitaji majadiliano ya kina na pia kuhusishwa kwa umma.

Kuria asema umaarufu wake katika ngome ya Raila uko juu

Waziri wa Viwanja, biashara na uwekezaji, Moses Kuria ameendelea kutetea hatua yake ya kusema kwamba ataruhusu uagizwaji wa gunia milioni 10 za mahindi ya GMO kuja humu nchini ili kuwasitiri Wakenya wanaokufa njaa.

Baada ya matamshi yake hivi majuzi kuwa Wakenya huwa wanakufa kila mara na kuna vitu vingi vinavyohatarisha maisha na kwamba kuongeza mahindi ya GMO katika orodha hiyo si tatizo, sehemu ya Wakenya haswa viongozi kutoka mrengo wa upinzani wamekuwa wakipinga kauli hiyo na hata kumtaka Kuria kuomba wakenya msamaha kwa matamshi kama hayo.

Jumapili mchana kiongozi wa Azimio la Umoja One Kenya Raila Odinga alimtaka Kuria kuomba radhi na pia kusitisha hatua hiyo ya kuruhusu mahindi ya GMO kuja humu nchini kama njia ya kupiga njaa vita.

Kulingana na bwana Raila, suala la GMO si jambo la kukurupukiwa tu hivi bali linahitaji majadiliano ya kina na pia kuhusishwa kwa umma kwa sababu hatari za GMO kiafya ni nyingi na zinafaa kujadiliwa hadharani.

Kuria amejibu vikali huku akisema kwamba wale wote wanaopinga kuagizwa kwa mahindi ya GMO watafia jehanamu kwani wengi wao wana vyakula vya kuwasitiri na wanapinga GMO ambayo yanafaa kuja kama suluhisho kwa makali ya njaa inayowakumba mamilioni ya Wakenya katika sehemu mbalimbali.

“Haifai kabisa kwa wavivu matajiri nwa kuTwitterati huku wakiwa na bakuli la pizza na vijisamaki kuendelea kushambulia sera yetu ya GMO huku Hustlers wakifa kwa njaa na nyama ya punda yenye sumu. Mtaungua kuzimu,” Kuria alisema kupitia ukurasa wake wa Twitter.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved