logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alinur azungumzia video ya mwanahabari akichapwa na walinzi wa mkewe DP Rigathi

Ugomvi huo ulisuluhishwa na afisa wa polisi, kama inavyoonekana kwenye video.

image
na Radio Jambo

Habari24 November 2022 - 10:17

Muhtasari


  • Huku mwanasiasa na mfuasi sugu wa muungano wa azimio akizungumzia suala hilo alisema kwamba uhuru hatimaye umekuja kwa watu Wakenya

Mwanahabari mmoja ameripotiwa kushambuliwa kimwili na maafisa wa usalama wanaohusishwa na mkee naibu rais Dorcas Rigathi wakati wa ugawaji wa chakula cha msaada ambao aliutayarisha huko Gatanga, kaunti ya Murang'a.

Mwanahabari huyo ambaye anasemekana kuwa mwanahabari wa Daily Nation katika kaunti hiyo, aliripotiwa kuchomoa simu yake ya rununu ili kurekodi maudhui ya jukwaa la kidijitali.

Mara tu baada ya kumrekodi mkewwe naibu Rais Dorcas, maafisa wake wa usalama walimvamia na kumkashifu.

Ugomvi huo ulisuluhishwa na afisa wa polisi, kama inavyoonekana kwenye video.

Huku mwanasiasa na mfuasi sugu wa muungano wa azimio akizungumzia suala hilo alisema kwamba uhuru hatimaye umekuja kwa watu Wakenya.

Wakenya wengi waliona matamshi yake Alinur yakiwa kejeli.

"Mwanahabari kutoka Kaunti ya Murang'a kwa jina Mwangi Muiruri akipigwa na maafisa wa usalama wanaohusishwa na mke wa Naibu Rais Rigathi Gachagua, Madam Dorcas Rigathi. Haya yalijiri wakati wa hafla ya usambazaji chakula cha msaada huko Gatanga, kaunti ya Murang'a. Uhuru uko hapa watu wangu."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved