logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kijana wa miaka 17 akamatwa kwa kuwapachika wanawake 10 mimba

Wanawake zaidi ya 10 waliokolewa katika operesheni ya polisi, tayari wakiwa na mimba.

image
na Radio Jambo

Habari14 January 2023 - 05:10

Muhtasari


• Wanawake zaidi ya 10 waliokolewa katika operesheni ya polisi, tayari wakiwa na mimba.

• Kiwanda hicho haramu cha kuzalisha watoto kwa ajili ya kibiashara kilivamiwa na polisi baada ya kudokezewa na wananchi.

Mwanaume aliyekamatwa

Mvulana mwenye umri wa miaka 17 kwa jina Noble Uzuchi anaripotiwa kuzuiliwa na Polisi nchini Nigeria kwa kuwapa ujauzito wanawake zaidi ya 10.

Kulingana na chombo cha habari cha Nigeria, PUNCH, Kamandi wa Polisi wa Jimbo la Rivers nchini Nigeria alifichua na kuzima operesheni ya kiwanda cha watoto katika maeneo ya serikali ya mitaa ya Obio/Akpor na Ikwerre jimboni humo.

Washukiwa wanne wamekamatwa kuhusiana na operesheni hiyo haramu na wasichana kumi wajawazito wameokolewa.

Kulingana na polisi, Uzuchi na Chigozie Ogbonna mwenye umri wa miaka 29 waliajiriwa na kundi hili ambalo lilifungua kiwanda cha kuzalisha watoto kwa ajili ya kibiashara.

“Kiongozi wa harambee hiyo, Peace Alikoi mwenye umri wa miaka 40, basi angehifadhi watoto na kuwalipa akina mama kiasi cha N500,000 (KES 138,406). Baadhi ya watoto wachanga pia waliuzwa. Polisi pia wamemkamata Favour Bright mwenye umri wa miaka 30 kuhusiana na operesheni hiyo,” Punch waliripoti.

Polisi walidokezwa kuhusu operesheni hiyo na kuchukua hatua haraka kutokana na taarifa hiyo na kuvamia nyumba mbili za jamii ya Igwuruta na Omagwa ambako waathiriwa walikuwa wamehifadhiwa.

Wahasiriwa ambao wengi wao walikuwa wajawazito waliokolewa na kuwekwa chini ya ulinzi kwa uchunguzi zaidi. Polisi pia wamelipata gari aina ya Honda Pilot Jeep kutoka kwa kiongozi wa harambee hiyo.

"Waathiriwa wote walikiri kwamba walishawishiwa kwa mauzo haramu ya watoto kwa sababu ya hitaji la kukabiliana na baadhi ya changamoto za kifedha," Iringe-Koko, mratibu wa polisi aliiambia Punch.

Kesi hiyo imehamishiwa katika Idara ya Upelelezi wa Jinai ya Serikali na juhudi zinaimarishwa kuwasaka na kuwakamata wanunuzi wa watoto ambao tayari wameuzwa.

"Hatutapumzika hadi wale wote waliohusika katika kitendo hiki kiovu wafikishwe mahakamani na kuwajibishwa kwa matendo yao," Iringa-Koko aliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved