logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kisii:Mwanafunzi wa chuo akamatwa kwa kuendesha duka feki la Jumia, kulaghai watu mamilioni

Mlaghai huyo alipatikana na laini 22 za simu kabla ya kuelekeza polisi kwa wenzake Kiambu.

image
na Radio Jambo

Burudani16 January 2023 - 07:40

Muhtasari


• DCI walisema kuwa mwanafunzi huyo na wenzake walikuwa wanauza bidhaa hewa kwa ofa ya Krismasi na mwaka mpya.

Mlaghai huyo alikuwa anaendesha ukurasa feki wa Jumia

Walaghai watatu mashuhuri walikamatwa mwishoni mwa juma kwa kujipatia pesa kutoka kwa watu kwa njia ya ulaghai, kwa kutumia majukwaa ya uwongo ya mtandaoni yanayodaiwa kuuza bidhaa.

Kulingana na taarifa na kitengo cha ujajusi DCI,  nwatatu hao ni pamoja na Dickson Magembe, Dionicious Omonyi na Derrick Kodek walikamatwa kwa kishindo na maafisa, kufuatia malalamiko mengi yaliyopokelewa kutoka kwa umma kupitia mitandao ya DCI ya Facebook na Twitter.

Watatu hao wanaaminika kujipatia mamilioni ya pesa kutoka kwa wanunuzi ambao hawakutarajia, kwa kuendesha akaunti ghushi wakiiga maduka maarufu ya mtandaoni ya JUMIA.

Kupitia ukurasa ghushi wa Facebook ‘Jumia Shopping’ watatu hao waliendesha promosheni katika kipindi cha Krismasi na Mwaka Mpya ikitoa punguzo la hadi 40% kwa bidhaa mbalimbali za nyumbani, na kuvutia wanunuzi wengi bila kutarajia.

Nambari ya till ya MPESA ambapo amana zingewekwa kabla ya kuwasilisha bidhaa na baada ya malipo kufanikiwa, ankara itatumwa kupitia WhatsApp ikiahidi kutumwa bila malipo ndani ya saa 24.

Hiyo ingeashiria mwisho wa mawasiliano kwani wateja wenye hamu wangeblockiwa kote mitandaoni, na kuwaacha wakiwa wamekata tamaa na hasara kubwa ya kubeba.

DCI waliripoti kuwa walaghai hao walimuibia mtu mmoja kutoka kaunti ya Tharaka Nithi kiasi cha karibia laki moja kabla ya kumzimia simu na kokatisha mawasiliano naye kote mitandaoni.

“Haya yalimtokea mwathiriwa huko Mukothima, Kaunti Ndogo ya Tharaka Kaskazini, ambaye alilipa Sh 95,000 kwa kiti cha viti 7 na meza ya kahawa. Hii ni baada ya ofa kutolewa kwenye ukurasa ghushi wa Facebook ikitangaza punguzo la 40% kwa viti vya kuegemea na vitu vingine vya nyumbani,” DCI waliripoti.

Baada ya kuwatia nguvuni, polisi walipata laini za simu zipatazo 22 ambapo mmoja wa wezi hao ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Kisii akisoma mwaka wa 3.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved