logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwili wafukuliwa baada ya mwezi na kukutwa umegeuzwa ukiwa bila sanda!

Mtoto huyo alizikwa mwezi mmoja uliopita lakini kaburi lake likaonekana kuhitilafiwa.

image
na Radio Jambo

Makala20 March 2023 - 09:29

Muhtasari


• Baada ya kufukuliwa kwa kaburi, mtoto huyo alipatikana lakini hakukuwa na sanda na mwili wake ulikuwa umegeuzwa.

• Wakaazi hao walisema vitendo vya watu kupatikana na viungo vya mwili si jambo geni katika eneo hilo.

Mwili wafukuliwa na kuutwa umegeuzwa.

Familia moja imepigwa na butwaa baada ya kufukua kaburi la mpendwa wao na kukuta mwili umegeuzwa kinyume na walivyousitiri awali wakati wa maziko.

Tukio hilo lilijiri katika mkoa wa Geita nchini Tanzania ambapo baada ya malalamishi kutoka kwa wanafamilia ambao walidai kwamab kaburi la mpendwa wao mtoto lilikuwa na ishara ya kuhitilafiwa, walitaka kibali ili kufukua na kuhakikisha iwapo mwili huo upo kaburini au umeibwa.

Mtoto huyo marehemu alizikwa mwezi uliopita lakini baada ya siku chache, familia ikazua madai kwamba kaburi hilo lilionekana kuhitilafiwa na wikendi iliyopita baada ya mamlaka husika kutoa kibali cha kufukuliwa kwa hakiisho, wanafamilia kwa kushirikiana na mamlaka walianzisha shughuli ya kuufukua mwili wake.

Baada ya kuufukua, waliukuta mwili huo ukiwa ndani ya jeneza kama ambavyo waliusitiri hapo awali lakini butwaa waliyokumbana nayo ni kwamba mwili huo ulikuwa umegeuzwa, kulingana na wale waliousitiri kipindi cha kumpa buriani.

“Baada ya kwamab tumefungua lile jeneza, tulikuta mwili umo lakini umegeuzwa. Lakini sanda hatukuiona. Sanda hatukuiona kwa uzuri, tuliona mwili umo, kichwa kimo na viungo vingine vimo. Lakini ni jambo ambalo limekuwa likitishia Amani sana,” Lucas Madaha ,mmoja wa wanafamilia waliokuwa katika kuuandaa mwili huo na sambamba katika kuufukua alisema.

Wakaazi hao walisema tukio la kuukuta mwili umegeuzwa liliwapiga butwaa pakubwa kwani hawajui kilichotokea kufuatia wasiwasi wa Imani za kishirikina zilizotokea katika kaburi la mtoto huyo.

Wakaazi hao walisema vitendo vya watu kupatikana na viungo vya mwili si jambo geni katika eneo hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved