logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mike Sonko awashauri 'side chicks' kuwa na subira na waume wao

Viongozi kadhaa wa dunia akiwemo rais wa Kenya William Ruto walihudhuria hafla hiyo.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 May 2023 - 15:00

Muhtasari


  • Mamilioni ya watu walifuatilia tukio hilo kote ulimwenguni. Tukio hili limepangwa kwa zaidi ya miezi minane.
Aliyekuwa gavana wa Nairoi, Mike Sonko

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko amewashauri mipango wa kando kuwa na subira na wanaume wao.

Aliwahimiza kushikamana na wanaume wao na sio kuwaacha.

Mike Sonko alikuwa akimrejelea Camila ambaye ni mke wa Mfalme Charles.

Mfalme mpya wa Uingereza alitawazwa leo(Jumamosi) katika hafla ya kimataifa iliyohudhuriwa na viongozi wa ulimwengu.

Camila alikuwa mpenzi wa Mfalme Charles kwa miaka mingi. Walianza kuchumbiana hata wakati Charles alikuwa bado amemuoa na Princess Diana. Baadaye walifunga ndoa mnamo 2005.

Mfalme Charles alitawazwa katika sherehe ya kupendeza huko London.

Mfalme anachukua nafasi ya mamake Malkia Elizabeth aliyefariki mwaka jana. Alikuwa mfalme aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi katika historia ya Uingereza.

Viongozi kadhaa wa dunia akiwemo rais wa Kenya William Ruto walihudhuria hafla hiyo.

Mamilioni ya watu walifuatilia tukio hilo kote ulimwenguni. Tukio hili limepangwa kwa zaidi ya miezi minane.

Sonko alisema;

"KWA WOTE SIDE CHICS. Ninataka tu kukuhimiza popote ulipo, amini tu na kuwa mwaminifu kwa wanaume wako. Leo, mwenzako/aliyekuwa chic, Camila ni Malkia Consort wa Uingereza. She was Prince Charles' side chic ambaye baadae alifunga ndoa rasmi na Prince mwaka wa 2005 baada ya marehemu Princess Diana kuanza kuhangaika na kupigwa mangwa na kupigwa ma quickie mpaka kwa magari."

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved