logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanawake ndio kivutio kikuu cha utalii Kenya, acha kutoza vipodozi ushuru - MP Owino

Owino alisema serikali kutoza ushuru bidhaa za urembo ni sawa na kuwaibia wanawake.

image
na Radio Jambo

Makala11 May 2023 - 09:01

Muhtasari


• "Kivutio cha kipekee kwa watalii humu nchini ni wasichana wetu warembo. Kwa hiyo Kenya itapoteza mabilioni ya dola kwa sababu watalii watakoma kuja huku,” - Owino.

Babu Owino aikosoa serikali kutoza bidhaa za urembo ushuru.

Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino ameisuta serikali ya Kenya Kwanza kwa hatua ya kutaka kutoza ushuru kwa bidhaa za urembo.

Owino alisema kuwa hatua hiyo ni sawa na kuwaibia watoto wa kike kwani asilimia kubwa ya bidhaa za urembo hutumiwa na wanawake.

“Serikali imepoteza mwelekeo, sasa inatoza ushuru kwa kila kitu. Sasa hivi wanatoza ushuru kwa mawigi, rangi za kucha, na hata ndevu bandia, vitu vyote ambavyo vinafanya vijana wetu kurembeka. Serikali ambayo inaiba kutoka kwa mabinti zetu si serikali nzuri. Mwanamume kamili hafai kuibia wanawake,” Owino alisema.

 Mbunge huyo mkereketwa wa sera za ODM alimsuta vikali rais Ruto akisema kuwa hatua hiyo itaifanya Kenya kupoteza mapato makubwa kutokana na sekta ya utalii kwani wanawake ndicho kivutio kikubwa cha utalii kwa sababu ya kupendeza kwao.

“Mabinti zetu wanavalia hizi bidhaa za urembo ili kuvutia watalii. Kivutio cha kipekee kwa watalii humu nchini ni wasichana wetu warembo. Kwa hiyo Kenya itapoteza mabilioni ya dola kwa sababu watalii watakoma kuja huku,” Owino alielezea.

Wiki jana wizara ya fedha ilitoa pendekezo kutaka bidhaa za urembo kuongezewa ushuru kama njia moja ya kuongeza pato la kitaifa ili kukidhi bajeti ya serikali, hatua ambayo hata hivyo imepata pingamizi kali kutoka kwa sehemu ya Wakenya ambao wanasema ushuru huo ni mzigo mzito kwa wananchi ambao tayari wamelazimika kubeba mzigo mzito wa ushuru katka bidhaa mbalimbali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved