logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto, DP Gachagua wainuka na kunyenyekea wakimsalimia Raila Odinga

Raila alipofika, alielekea kwenye jeneza la Mukami na kutoa heshima yake kwake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri13 May 2023 - 09:17

Muhtasari


• Ruto na Gachagua walitangulia kufika katika hafla hiyo huko Nyandarua na Odinga alifika nyuma.

• Raila alimsalimia Naibu Rais Rigathi Gachagua na kumwendea Rais mashuhuri William Ruto.

• Ruto aliinuka kupeana naye mkono huku umati ukishangilia.

Ruto na Rigathi wainuka na kunyenyekea kumsalimia Raila Odinga katika mazishi ya Mukami Kimathi.

Kwa mara ya kwanza rais William Ruto na naibu wake Rigathi Gachaua wamekutana uso kwa uso na 'mbaya' wao wa kisiasa Raila Odinga na kusalimiana naye hadharani.

Watatu hao walikutana katika hafla ya kumpa buriani marehemu Mukami Kimathi ambaye alikuwa mmoja wa wanachama wa Mau Mau - kundi la mashujaa waliopigania uhuru wa Kenya kutoka kwa wakoloni kati ya mwaka 1952 hadi 1963.

Ruto na Gachagua walitangulia kufika katika hafla hiyo huko Nyandarua na Odinga alifika nyuma na kuelekea kwenye jeneza la Mukami na kutoa heshima yake kwake.

Kisha akaendelea hadi kwa viongozi waliokuwepo.

Raila alimsalimia Naibu Rais Rigathi Gachagua na kumwendea Rais mashuhuri William Ruto.

Ruto aliinuka kupeana naye mkono huku umati ukishangilia.

Mazishi ya Mukami yalishuhudia Ruto na Raila wakikutana kwa mara ya kwanza baada ya uchaguzi mkuu wa 2022 uliokuwa na ushindani mkali.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Ruto, Gachagua na Raila kukutana ana kwa ana.

Viongozi hao wamekuwa wakirushiana vijembe hadharani kuhusu gharama ya maisha, Mswada wa Sheria ya Fedha, 2023, maandamano, sakata ya Shakahola, uteuzi wa serikali miongoni mwa masuala mengine.

Raila ni miongoni mwa viongozi wakuu walioshiriki ibada ya mazishi.

Raila alikuwa amethibitisha kuwa atahudhuria ibada ya mazishi.

“Siwezi kukosa mazishi ya Shujaa Mama Mukami wa Kimathi. Tumekuwa karibu sana na nitakuwa Njabini kwa sherehe yake ya mwisho duniani,” Raila alisema.

Mukami Kimathi alifariki akiwa na umri wa miaka 96 alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Nairobi baada ya kupata matatizo ya kupumua.

Aliaga dunia Alhamisi usiku, Mei 4, 2023


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved