logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneta Ledama Olekina ampa kazi msichana jasiri aliyewasuta viongozi Uasin Gishu

“Mercy Tarus Ningependa unifanyie kazi… sema moyo wako" Olekina.

image
na Radio Jambo

Burudani10 August 2023 - 08:29

Muhtasari


• Kuwasuta kwake mbele ya macho yao kuliwavutia Wakenya wengi kwa jinsi msichana huyo mhitimu alivyowapa makavu ana kwa ana bila kuwaficha.

• Mercy Tarus ni miongoni mwa vijana wahitimu ambao walirambwa kwenye skendo kubwa.

Olekina kumpa kazi Mercy Tarus

Seneta wa Narok Ledama Olekina amejitokeza na kusema kwamba yuko tayari kukutana na binti Mercy Tarus ili kumpa kazi.

Mercy Tarus mapema wiki hii aligonga vichwa vya habari baada ya kuwasuta vikali viongozi wa kaunti ya Uasin Gishu – seneta wa sasa ambaye ni gavana wa zamani Jackson Mandago, gavana wa sasa Jonathan Bii Chelilim na naibu gavana Barorot miongoni mwa wengine.

Kuwasuta kwake mbele ya macho yao kuliwavutia Wakenya wengi kwa jinsi msichana huyo mhitimu alivyowapa makavu ana kwa ana bila kuwaficha.

Ni kutokana na ari hii ambapo seneta Olekina amejitolea kumpa kazi akisema kwamba kesho angavu ni ya vijana wenye ujasiri kama wa kwake.

“Mercy Tarus Ningependa unifanyie kazi… sema moyo wako … wakati ujao ni wa vijana waaminifu! Hebu tuzungumze,” Olekina alimwambia kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Mercy Tarus ni miongoni mwa vijana wahitimu ambao walirambwa kwenye skendo kubwa ambayo imekuwa ikizua mjadala mkali mitandaoni na amabyo ilifanyika katika kaunti ya Uasin Gishu chini ya uongozi wa seneta wa sasa.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, kaunti hiyo iliwahadaa wqzazi kutoa mamilioni ya pesa kwa ajili ya serikali kuwasaidia katika kuwapeleka wanao kujiendeleza kimasomo nchini Ufini, lakini hilo halikutokea, na wachache waliokwenda Ufini waliishia kuhangaika na kufukuzwa masomoni kwa kutolipiwa ufadhili wa masomo kama ambavyo kaunti ilivyowaambia wazazi.

Katika video moja, msichana huyo alionekana akiwauliza maswali magumu viongozi hao ambao walifika katika mkutano uliowakutanisha wazazi wahanga na watoto wao, katika mbinu na kutafuta suluhisho la kudumu kwa sakata hilo ambalo sasa limeenea pakubwa hadi nje ya nchi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved