logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pasta ajitupa kutoka ghorofani na kufa baada ya mrembo aliyemsomesha chuo kikuu kumkataa

"Aliruka chini kutoka kwa jengo la ghorofa mbili na kufa."

image
na Radio Jambo

Habari28 August 2023 - 06:25

Muhtasari


• Kulingana na utamaduni wa kijiji chao, jamaa huyo alisema alizikwa msituni kwa kufanya “kufuru”.

Mchungaji mmoja wa Kanisa la Kipentekoste nchini Nigeria amejiuwa kwa kujirusha kutoka juu ya ghorofa kisa mgogoro wa kimapenzi.

Kwa mujibu wa jarida la Punch nchini humo, mchungaji huyo mwenye umri wa miaka 30 aliyetambulika kwa jina moja kama Prosper alijitupa kutoka juu ya jengo la Ghorofa mbili na kufariki papo hapo baada ya kuachwa na mpenzi wake, ambaye alikuwa ametumia muda mwingi kumgharamikia.

Jamaa wa marehemu ambaye alizungumza na wanahabari siku ya Jumamosi, alisema mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 30 alimfundisha mpenzi wake katika chuo kikuu, ambapo alikataa ombi lake la ndoa.

Alisema, “Tukio hilo lilitokea mwezi uliopita. Mwanamume huyo (Igboke) alikuwa na umri wa miaka 30 wakati wa kifo chake. Mpenzi wake ambaye alikusudia kumuoa alimkatisha tamaa baada ya kumaliza kumsomesha chuo kikuu.

"Aliruka chini kutoka kwa jengo la ghorofa mbili na kufa. Ninashangaa kwamba mwanamume wa umri huu na mchungaji anaweza kufanya hivi.”

Kulingana na utamaduni wa kijiji chao, jamaa huyo alisema alizikwa msituni kwa kufanya “kufuru”.

"Hatimaye alizikwa Ijumaa kwenye kichaka katika jamii yake," chanzo kiliongeza.

Visa vya wanaume kujitoa uhai baada ya kutendwa unyama na wapenzi wao waliowahudumia kwa hali na mali si vigeni kutembea, na ni muda tu baada ya wanaume kujifuzna kutokana na matukio kama hayo ya awali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved