logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mganga wa kienyeji na mkewe mbaroni baada ya mgonjwa kufariki kilingeni

Enanga alisema washukiwa hao wawili wanakabiliwa na mashtaka yanayohusiana na uzembe

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 August 2023 - 05:57

Muhtasari


• Alibainisha kuwa hali ya Nantale ilizidi kuzorota, mganga huyo na mkewe walikataa kumpeleka hospitalini.

Polisi katika wilaya ya Bugweri mashariki mwa Uganda wamemkamata mganga mmoja na mkewe baada ya mwanamke mmoja ambaye aliletwa katika kilinge chao kwa matibabu kufariki, jarida la Nile Post limeripoti.

 Kulingana na msemaji wa polisi nchini humo, Fred Enanga, Bateganya Bwiga, 62 alikamatwa pamoja na mkewe, Madina Baseke, 70 baada ya Margaret Nantale, 53 kufariki katika kilinge chao katika kijiji cha Budubye, kata ndogo ya Buyanga wilayani Bugweri.

"Mganga wa kienyeji alisababisha uhamisho wa Nantale kutoka kwa kilinge cha Obara hadi kwenye kilinge chake na kumhudumia kwa siku tatu. Waliendelea kumzuilia mwathiriwa katika kilinge chao hata hali yake ilipokuwa mbaya badala ya kumpeleka hospitali kwa matibabu zaidi,” Enanga alisema.

Alibainisha kuwa hali ya Nantale ilizidi kuzorota, mganga huyo na mkewe walikataa kumpeleka hospitalini kwa matibabu bali walimweka kwenye kilinge chao kwa siku tatu hadi alipofariki.

Enanga alisema washukiwa hao wawili wanakabiliwa na mashtaka yanayohusiana na uzembe wa uhalifu na kusababisha kifo cha mtu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved