Wachaneni na hii dialogue-Raila aambiwa

Wakati uo huo viongozi wa Azimio wakiongozwa na Odinga walikutana na kufanya waandishi wa habari na kuionya serikali ya Ruto dhidi ya kuongeza bei ya petroli

Muhtasari
  • Njiru alisisitiza kwamba hastlas wamechoka na kwamba wako tayari kufanya lolote ambalo Raila Amollo Odinga atawaambia.
Gachagua amshambulia Odinga tena
Gachagua amshambulia Odinga tena
Image: Maktaba

Ndegwa Njiru ni Wakili wa Kenya wa Mahakama Kuu. Yeye ni wakili anayejulikana na Wakenya wengi kwa sababu amekuwa akiwakilisha wanasiasa wenye nguvu katika kesi mahakamani.

Ndegwa Njiru amewaambia viongozi wa Azimio La Umoja One Kenya Alliance wakiongozwa na Raila Amollo Odinga, Stephen Kalonzo Musyoka, Martha Karua, Jeremiah Kioni na Eugene Wamalwa kwamba wanapaswa kusitisha Mazungumzo ya Kitaifa na serikali ya Muungano wa Kenya Kwanza inayoongozwa na Rais William Samoei Ruto.

Njiru alisisitiza kwamba hastlas wamechoka na kwamba wako tayari kufanya lolote ambalo Raila Amollo Odinga atawaambia.

Njiru alizungumza hayo baada ya Wakenya wengi kuanza kulalamikia Mamlaka ya Nishati ya Petroli na Udhibiti EPRA kupandisha bei ya mafuta ya petroli kama vile Petroli, Dizeli na Taa jana.

"Wachaneni na hii DIALOGUE we hit the road running....ardhi imeiva kwa kukimbia...ardhi imeiva...imeiva hadi kiini...HUSTLERS are ready uwezo na nia.. @RailaOdinga@skmusyoka@MarthaKarua@HonKioni@EugeneLWamalwa,"Ndegwa aliandika.

Wakati uo huo viongozi wa Azimio wakiongozwa na Odinga walikutana na kufanya waandishi wa habari na kuionya serikali ya Ruto dhidi ya kuongeza bei ya petroli, Dizeli na Mafuta taa kila mwezi.