logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Piga magoti mbele ya Raila, omba msamaha - Eric Omondi amshauri Jalang'o

Alisema hataki hali ya mbunge huyo kuachia kiti cha Lang’ata kwa kuwa atakuwa amemwangusha.

image
na

Yanayojiri23 September 2023 - 12:21

Muhtasari


• Alipoulizwa iwapo atawania kiti cha Lang'ata iwapo Jalang'o atatimuliwa, alisema sauti ya watu ni sauti ya Mungu.

• Alisema hataki hali ya mbunge huyo kuachia kiti cha Lang’ata kwa kuwa atakuwa amemwangusha.

Eric Omondi na Jalang'o

Mcheshi Eric Omondi amemshauri Mbunge wa Langáta Phelix Odiwuor almaarufu Jalangó kwenda kumwomba msamaha kiongozi wa Azimio la Umoja Raila Odinga.

Katika mahojiano na kituo kimoja cha redio mnamo Ijumaa, Omondi aliambia Jalang'o pia kuomba msamaha kwa wakazi wa Lang'ata, chama cha ODM na Mungu.

“Ninachopenda kumshauri Jalang’o ni kwamba, aamke mapema, ajiandae, ale kifungua kinywa, aingie kwenye gari lake na kuelekea kwa Baba Raila Amollo Odinga, apige magoti mbele yake na kuomba msamaha,” alisema.

"Baada ya hapo, anafaa kurejea bungeni, kuomba msamaha kutoka kwa wapiga kura na kisha kuelekea kanisani ili aombe msamaha kwa Mungu pamoja na wanachama wa ODM."

Omondi alisema ikiwa Jalang'o hataenda mbele ya wale anaopaswa kuwaomba msamaha, basi asahau kuhusu kufanikiwa.

Alipoulizwa iwapo atawania kiti cha Lang'ata iwapo Jalang'o atatimuliwa, alisema sauti ya watu ni sauti ya Mungu.

Alisema hataki hali ya mbunge huyo kuachia kiti cha Lang’ata kwa kuwa atakuwa amemwangusha.

"Tatizo langu kubwa kwa sasa sio Lang'ata bali ni Rais William Ruto. Kwa kawaida huwa nawaambia watu kwamba kuhusu lang'ata, sauti ya watu ni sauti ya Mungu. Sauti zote nimekuwa nikisikia kuhusu mimi kuwania nafasi hiyo." kiti si sauti yangu bali ni ya Mungu


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved