logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kizaazaa kanisani fundi wa majeneza akimsihi pasta kuombea biashara yake kushamiri

Alipotamka kwamba anataka biashara ya kuuza majeneza inawiri, mchungaji alipigwa na mshangao.

image
na Radio Jambo

Makala25 September 2023 - 10:17

Muhtasari


• Mwanamume huyo seremala alijongea kwa unyenyekevu mbele ya madhabau akiwa tayari na ombi lake.

• "Amekwenda kanisani akamwambia pasta naomba uombee biashara yangu istawi kwa sababu biashara imedidimia sana,” sehemu ya ujumbe huo ilisomwa na mtangazaji.

Jeneza tupu.

Muumini wa kanisa moja humu nchini amewashangaza wasikilizaji wa kituo kimoja cha redio humu nchini baada ya kuhadithia tukio lililotokea katika kanisa anakoabudu.

Kwa mujibu wa ujumbe huo ambao ulisomwa hewani asubuhi ya Jumatatu Septemba 25, jamaa huyo ambaye ni fundi seremala wa kutengeneza majeneza alikwenda kanisani kwa ibada ya Jumapili kama kawaida.

Baada ya mahubiri, mchungaji aliwaita waumini weney uhitaji maalum kujongea kwenye madhabahu wakiwa na ombi ambalo wangependa mchungaji awafikishie kwa Mungu.

Mwanamume huyo seremala alijongea kwa unyenyekevu mbele ya madhabau akiwa tayari na ombi lake.

“Amekwenda kanisani akamwambia pasta naomba uombee biashara yangu istawi kwa sababu biashara imedidimia sana,” sehemu ya ujumbe huo ilisomwa na mtangazaji.

Mchungaji alijitolea kumuombea lakini mwanzo akamuuliza ni biashara gani ili kwamba aweke mambo sawa wakati anatuma ombi hilo kwa Mungu kulijibu.

Mtumishi wa Mungu alipigwa na butwaa baada ya fundi seremala kutamka waziwazi kwamba alikuwa anataka biashara yake ya kutengeneza na kuuza majeneza iombewe ili inawiri, kwa kile alisema kwamba katika siku za hivi karibuni imekuwa ikididimia kwa kukosa wateja – wafu.

“Wateja hawaji na sipati kipato cha kukimu mahitaji yangu kama iluivyokuwa hapo awali. Naomba uniweke kwa maombi biashara iinuke tena. Biashara yangu ni fundi wa majeneza,” alisema huku mchungaji akishtuka na kusita huku umati uliokuwa unaguna ukisita kwa kimya cha ghafla.

Watangazaji walichagiza katika ujumbe huo mmoja akijaribu kuiga jinsi mchungaji angeombea biashara ya muumini wa kanisa lake ili kupata faidia na baadae kurudisha shukrani ya fungu la kumi kwa Mungu baada ya biashara kushamiri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved