Mfanyikazi wa mochwari afutwa kazi kwa kufanya mapenzi na mdoli wa marehemu

Mhudumu huyo wa makafani alitumwa kuchukua mwili wa mtu aliyekufa katika nyumba yake kifo cha kawaida lakini alipoingia kwake, alivutiwa na mwanasesere aliyekuwemo mwenye ukubwa wa binadamu.

Muhtasari

• Ryan Smith, 41, alikamatwa Ijumaa kwa mashtaka ya wizi, uvunjaji wa sheria, na kuharibu ushahidi halisi.

• Smith kisha inadaiwa alitoka nje - nguo zake zikiwa zimechafuka - na kumuonya meneja kwamba angerudi na kibali cha kumnunua mwanasesere.

Chumba cha kuhifadhi maiti
Chumba cha kuhifadhi maiti
Image: BBC

Mfanyikazi wa makafani katika jimbo la Nebraska nchini Marekani alifutwa kazi wiki iliyopita baada ya kufumaniwa akishiriki ngono na mwanasesere wa ukubwa wa binadamu ambaye alikuwa wa maiti ambaye alipewa jukumu la kuusafirisha, polisi walisema kwa mujibu wa New York Post.

Ryan Smith, 41, alikamatwa Ijumaa kwa mashtaka ya wizi, uvunjaji wa sheria, na kuharibu ushahidi halisi - na alifukuzwa mara moja kutoka kwenye jukumu lake la kuhifadhi maiti katika makafani ya Omaha.

Smith alisemekana kutekwa hisia na mdoli huo baada ya kuuona ndani ya makazi ya Rock Creek Apartments ambapo yeye na mwenzake walitumwa kuchukua mwili wa mtu aliyekufa kifo cha kawaida, kwa mujibu wa nyaraka za mahakama zilizopatikana na WOWT, NYP walisema Zaidi.

Wawili hao walikuwa wakifanya kazi kwa niaba ya Mid America First Call, kampuni inayoondoa, kusafirisha, kuhifadhi maiti na kuchoma maiti.

Baadaye siku hiyo, Smith alidaiwa kumpigia simu meneja wa mali na kudai Ofisi ya Sheriff ya Kaunti ya Sarpy ilikuwa ikimrudisha kwenye kitengo kuchukua mdoli huyo ili aweze kupigwa kwa "biopsy" - ombi la kushangaza ambalo lilikataliwa mara moja.

Hapo ndipo alijichanga na kijipenyeza kwenda kwa nyumba ya marehemu kabla ya kufanya mapenzi na mdoli huo.

Meneja alijikwaa kwenye eneo la kutatanisha wakati akichunguza kelele zinazotoka ndani ya kitengo, ambacho kilikuwa kimefungwa na kusimikwa kwa mnyororo.

Smith kisha inadaiwa alitoka nje - nguo zake zikiwa zimechafuka - na kumuonya meneja kwamba angerudi na kibali cha kumnunua mwanasesere.

Tishio hilo lilithibitika kuwa baya kwa Smith; meneja aliita polisi na kuripoti fujo hiyo, akisema alikuwa na wasiwasi mfanyakazi wa makafani atarudi kuvunja na kuiba mali kutoka kwa ghorofa hiyo.