Mfahamu mrembo wa miaka 24 anayefanya kazi ya kutunza na kupodoa maiti

Anaosha miili, kuchana au kunyoa nywele zao, kuwavisha, na kuwapaka vipodozi kama njia ya kuirembesha kwa ajili ya safari ya ‘heshima za mwisho’.

Muhtasari

• Bi Walton alianza kama mwanafunzi wa masuala ya utunzaji maiti mnamo 2019.

• Alianza kufanya kazi kwa muda wote akiwa na umri wa miaka 21, huku pia akisomea sifa zake za uwekaji dawa.

Chumba cha kuhifadhi maiti
Chumba cha kuhifadhi maiti
Image: BBC

Mrembo mmoja mwenye umri wa miaka 24 kutoka nchini Uingereza amewashangaza wengi baada ya kukiri kwamba kazi inayomuingizia kipato ni ile ya kutunza na kupodoa maiti katika makafani – kuitayarisha kwa njia faafu kwa safari ya ‘heshima za mwisho’.

Mrembo huyo kwa jina Isabel Walton, hivi karibuni alizungumzia kazi hiyo yake kwa heshima iliyotukuka katika mahojiano na runinga ya BBC na kusema kwamba anaipenda na wala haogopi kutangamana na maiti kila siku, kwani limekuwa jambo la kawaida katika maisha yake.

Mwanahabari wa BBC alipoweka kando woga wake na kukausha damu kutia guu katika maeneo ya kazi ya Walton, kitu cha kwanza alibaini ni Kuwepo kwa harufu isiyo ya kawaida katika chumba cha kuhifadhia maiti cha baridi na cha kutayarishia maiti.

"Tumewasha mfumo wa uingizaji hewa, lakini watu hawajazoea kemikali tunazotumia. Ingawa mimi sioni chochote cha ajabu," anasema Bi Walton.

Kuwa meneja wa chumba cha kuhifadhia maiti si kazi ya kawaida kwa kijana wa miaka 24.

"Watu wanashangaa jinsi nilivyo mdogo na kuwa mwanamke," anasema, "kwa sababu bado ni tasnia inayotawaliwa na wanaume."

Bi Walton alianza kama mwanafunzi wa masuala ya utunzaji maiti mnamo 2019. Alianza kufanya kazi kwa muda wote akiwa na umri wa miaka 21, huku pia akisomea sifa zake za uwekaji dawa.

Akiwa mmoja wa watoto wachanga zaidi, "alikwama kama kidole gumba" kwenye kozi za mafunzo. Familia yake daima imekuwa ikimuunga mkono, lakini marafiki zake "walishangaa" alipowaambia kile angekuwa akifanya.

Lakini mbali na kuingiwa na hofu yoyote, Bi Walton anasema kuzungukwa na kifo na maiti kila wakati kumempa faraja. "Ninajua kwamba nitatunzwa ikiwa chochote kitatokea."

Hifadhi ya maiti ina hadi miili 80. Kila moja huhifadhiwa kwa wastani wa siku 15-20.

Watu wengi hufikiri kwamba mtu aliyekufa huwekwa tu ndani ya jeneza kabla ya mazishi, anasema Bi Walton, lakini yeye hutumia muda kuandaa miili ili wapendwa waweze kutazama au kutumia muda nayo kabla ya kuzikwa.

Anaosha miili, kuchana au kunyoa nywele zao, kuwavisha, na kuwapaka vipodozi kama njia ya kuirembesha kwa ajili ya safari ya ‘heshima za mwisho’.

"Ikiwa mtu amekuwa na hali mbaya kwa muda mrefu na amelazwa hospitalini, huenda familia hazijazoea kuwaona wakiwa na ndevu," asema Bi Walton.

"Wangetaka wavae vyema mavazi yao mazuri ya Jumapili na wawe safi kabisa kunyolewa na waonekane nadhifu tena."