Meru: Mke wa askofu ajeruhi nyeti ya mvulana, 17, akidai anatoka kimapenzi na bintiye, 15

Baada ya kuokolewa, inasemekana kijana huyo alipelekwa katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Meru kwa matibabu na kuruhusiwa kwenda nyumbani.

Muhtasari

• Brian anadai alipoteza fahamu baada ya kupigwa sana na mama, dada na kakake msichana huyo.

• Aliamka akiwa amefungwa kwenye mti huku suruali yake ikiwa imeshuka.

 

Image: BBC

Wakaazi wa kijiji cha Kiorimba kaunti ya Meru wamebaki na butwaa baada ya kubainika kwamba mke wa askofu mmoja katika eneo hilo alimshambulia vibaya kijana wa miaka 17 kwenye sehemu zake za siri.

Kwa mujibu wa ripoti kwenye runinga ya NTV Kenya, mke huyo wa askofu alimshambulia na kumjeruhi vibaya mvulana huyo kwa madai kwamba alikuwa anatoka kimapenzi na bintiye mwenye umri wa miaka 15.

Kulingana na Brian*, sio jina lake halisi, msichana huyo aligonga mlango wake saa 11 jioni kulala, lakini alikataa na kusisitiza kumsindikiza kurudi nyumbani kwa wazazi wake.

Alipofika nyumbani, alishambuliwa na watu wa familia ya msichana huyo.

Brian anadai alipoteza fahamu baada ya kupigwa sana na mama, dada na kakake msichana huyo.

Aliamka akiwa amefungwa kwenye mti huku suruali yake ikiwa imeshuka.

“Alichukua ile kamba na kunifunga kwenye sehemu zangu za siri na kuanza kubana kama unavyofanya unapochanua nguo baada ya kufua, nilihisi kuwa sehemu zangu za siri zinachanwa, nilipiga kelele za maumivu, sijui majirani. alisikia kilio changu,” alisema.

 

Baada ya kuokolewa, inasemekana kijana huyo alipelekwa katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Meru kwa matibabu na kuruhusiwa.

 

Wakaazi wamelaani tukio hilo na kutaka polisi kuchukua hatua.

 

Chifu wa eneo hilo Victoria Kimathi alithibitisha kisa hicho na kusema wanashirikiana na polisi kumtafuta mshukiwa huyo.