logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanawake wavamia ekari 10 za shamba la Miraa na kung'oa wakidai imeharibu wanaume wao

Pia waliharibu vilabu vya pombe na kuzichoma pombe zenyewe.

image
na Radio Jambo

Habari03 April 2024 - 09:52

Muhtasari


• " Sisi ni wajane kwa sababu ya hii muguka, wamekula wengine wakapatwa na saratani wakakufa juu ya sigara na hizi pombe, tumekataa sisi kama wanawake.”

Tanzania yateketeza shamba la miraa.

Makumi ya wanawake kutoka kijiji cha Oronie, kaunti ndogo ya Kajiado ya Kati kaunti ya Kajiado wamevamia shamba lenye ekari 10 za zao la miraa na kuiharibu kwa kuing’oa kwa ghadhabu katika kile wanadai mumea huo umewaharibia wanaume wao.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyopeperushwa kwenye runinga ya KBC1, wanawake hao walidai zao hilo limekuwa chanzo cha matatizo katika eneo lao, haswa kwa kuwaharibu wanaume ambao wamekuwa zuzu.

Wanawake hao pia walielekea katika kituo cha Enkorika kwenye kaunti hiyo ndogo na kufunga baadhi ya vilabu vya kuuza pombe kabla ya kuonekana wakiharibu pombe zenyewe kwa kupasua chupa na kuchoma.

“Sana sana chifu wa Orinie, atusaidie sababu tunaumia tukiwa wanawake. Sisi ni wajane kwa sababu ya hii muguka, wamekula wengine wakapatwa na saratani wakakufa juu ya sigara na hizi pombe, tumekataa sisi kama wanawake.”

“Tunaomba usaidizi wenu nyinyi kama serikali leo muingililie hili jambo lipate kutokomezwa hapa,” wanawake hao waliteta.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved