Corona yarejea kwa makali?

Hatari! Serikali yahofishwa na ongezeko la maambukizi ya Covid 19

Wengi wahofishwa na ongezeko la visa vipya

Muhtasari

 

  •  Mataifa  mengine yamerejesha masharti makali 
  • Wengi wamehofishwa na ongezko la visa vya maambukizi 
  • Kagwe amesema  janga litazuka endapo  hatua haitachukuliwa 

 

Waziri wa Afya Mutahi Kagwe

 Serikali imezua hofu kuhusu ongezeko la idadi ya visa vya covid 19 nchini.

Kupitia wizara  ya afya  ,serikali imesema ongezeko hilo limesababishwa na  ukiukaji wa kanuni zote zilizowekwa kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huo .

Waziri wa afya Mutahi Kagwe  amesema  kwa mfano baa haziwahitaji wateja wazo kuvalia maski au kutokaribiana .

Kagwe  amesema  mikusanyiko  ya watu katika mazishi ,harusi na mikutanoo ya kisiasa imerejelewa  huku kanuni zote zilizotolewa zikipuuzwa na wahusika .

 Hadi kufikia sasa Kenya imesajili visa  44,881  vya Covid-19  huku watu 685 wakipatikana na ugonjwa huo  siku ya jumapili .

" Tunahitaji kuangazia takwimu hizi na hasa ongezeko la visa vya wanaoambukizwa na vifo vinavyoripotiwa . Iwapo  hazimaanishi lolote basi  wajalini  wapendwa wenu  ..ni jukumu lenu kuwalinda’ amesema Kagwe .

Kagwe  amesema wakati rais Uhuru Kenyatta alipolegeza masharti hayo   kiwango cha maambukizi kilikuwa asilimia 4 lakini sasa kimezidi hadi asilimia 12 .

" Tunaweza kutabiri  patatokea janga  iwapo hatutachukua hatua za haraka ili kuzuia hili  tunaweza kuchagua kati ya kuzama ama kuogelea’ amesema Kagwe

 Kulingana na waziri Kagwe  watu katika umri wa kati ya miaka 20-39 ndio wanaosheheni asilimia 54 ya  visa vyote vya corona .

" Idadi kubwa ya walioaga dunia ni watu walio Zaidi ya umri wa miaka 58 lakini pia tumewapoteza watu walio na umri wa miaka 20 na 30  na leo wazazi wao wanalilia katika makaburi yao’ amesema