logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama yatoa waranti ya kukamatwa kwa gavana wa Kilifi Kingi

Watu wanne wanaoshtumiwa kwa jaribio la kumlaghai Kingi ni  George Ngugi, Abdul Aziz Alim, Moses Musee Maluki  na Noah Akala Aduwo.

image
na Radio Jambo

Habari21 October 2020 - 15:17

Muhtasari


  •  Watu wanne  hao  ni  George Ngugi, Abdul Aziz Alim, Moses Musee Maluki  na Noah Akala Aduwo.
  • Hakimu mkuu Eunice Nyutu ndiye aliyetoa waranti hiyo 

Mahakama moja jijini Nairobi imetoa waranti ya kukamatwa kwa gavana wa Kilifi Amason Kingi  kwa kukosa kuhudhuria kikao cha korti .

Kingi  alifaa kutoa ushahidi katika kesi ya uhalifu ambapo wafanyibiashara wane  wameshtakiwa kwa kujaribu kumlaghai shilingi milioni 30 .

 Hakimu mkuu Eunice Nyutu wa mahakama ya kupambana na ufisadi ya Milimani   pia ametoa waranti ya kukamatwa kwa   Ahemed Ibrahim,  shahidi wa upande wa mashtaka aliyekosa kwenda kortini  .Wawili hao wanafaa kukamatwa na kufikishwa kortini kwa maelekezo zaidi .

 Wakati kesi hiyo ilipofika kwenye ratiba ili kutajwa ,mwendesha mashtaka wa serikali alitaka waranti ya kukamatwa kwao itole2we kwa sababu hawaku mahakamani ili kutoa ushahidi wao .

 Watu wanne wanaoshtumiwa kwa jaribio la kumlaghai Kingi ni  George Ngugi, Abdul Aziz Alim, Moses Musee Maluki  na Noah Akala Aduwo.

 Wane hao ambao ni wafanyibiashara mjini Mombasa  wamekanusha mashtaka dhidi yao .

 Wanadai kujitambulisha kwa Kingi kama maafisa kutoka tume  ya EACC na kwamba walikuwa wakichunguza kesi ya ufisadi dhidi ya Gavana Kingi .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved