logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru awaacha hoi wakaazi wa Kisumu kwa kutua bandarini badala ya uwanja wa ndege wa Kisumu

Rais alikaribishwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga ,gavana wa Kisumu Anyang Nyong'o, naibu wake Matthews Owili na viongozi wengine waliochaguliwa

image
na Radio Jambo

Habari21 October 2020 - 15:31

Muhtasari


  •  Atazuru miradi mbali mbali inayoendelea katika kaunti hiyo
  • Amekuwa Kisii kupokea ripoti ya BBI 

Rasi uhuru Kenyatta siku ya jumatano  alitua kwa ghafla katika bandari inayokarabatiwa kwa kima cha shilingi bilioni 3 ya Kisumu .

 Rais alitarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Kisumu ambako wakaazi walikuwa wamemngoja huku wapiga ngoma na wanadensi wakitarajia kumlaki .

 Hata hivyo ndege yake ilionekana ikitua katika banadari ya Kisumu na kuwaacha na mafadhaiko wakaazi waliopiga foleni kando ya barabara ya Obote  na ile ya Oginga Odinga ili kumpokea

Uhuru  baadaye alielekea katika Ikulu ndogo  ya Kisumu . Rais alikaribishwa na  kiongozi wa ODM Raila Odinga  ,gavana wa Kisumu  Anyang Nyong'o,  naibu wake  Matthews Owili  na viongozi wengine waliochaguliwa .

 Siku ya alhamisi  Uhuru atakagua  ujenzi unaoendelea wa shilingi bilioni 1.4 wa uwanja wa michezo wa  Jomo Kenyatta International Stadium huko  Mamboleo kisumu mashariki .

 Pia atazuru  eneo la kibiashara Uhuru Business Park linalojengwa kwa kima cha shilingi milioni 350 na  kituo cha kustarehe cha  Jaramogi Oginga Odinga


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved