- Atazuru miradi mbali mbali inayoendelea katika kaunti hiyo
- Amekuwa Kisii kupokea ripoti ya BBI
Rasi uhuru Kenyatta siku ya jumatano alitua kwa ghafla katika bandari inayokarabatiwa kwa kima cha shilingi bilioni 3 ya Kisumu .
Rais alitarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Kisumu ambako wakaazi walikuwa wamemngoja huku wapiga ngoma na wanadensi wakitarajia kumlaki .
Hata hivyo ndege yake ilionekana ikitua katika banadari ya Kisumu na kuwaacha na mafadhaiko wakaazi waliopiga foleni kando ya barabara ya Obote na ile ya Oginga Odinga ili kumpokea
Uhuru baadaye alielekea katika Ikulu ndogo ya Kisumu . Rais alikaribishwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga ,gavana wa Kisumu Anyang Nyong'o, naibu wake Matthews Owili na viongozi wengine waliochaguliwa .
Siku ya alhamisi Uhuru atakagua ujenzi unaoendelea wa shilingi bilioni 1.4 wa uwanja wa michezo wa Jomo Kenyatta International Stadium huko Mamboleo kisumu mashariki .
Pia atazuru eneo la kibiashara Uhuru Business Park linalojengwa kwa kima cha shilingi milioni 350 na kituo cha kustarehe cha Jaramogi Oginga Odinga