Uchawi sishiriki!

Uchawi tena? Amber Ray ajitetea baada ya picha yake akiwa kwa ‘mganga’ kutolewa

Amber Ray kajipata mashakani

Muhtasari

 

  • Picha ya Amber akiwa amebeba kuku wawili yamtia mashakani 
  • Amejitetea lakini wengi hawamuamini 

 

Faith Makau  aayejulikana kwa mashabiki wake kama Amber Ray amejipata katika ndimi za wengi hivi karibuni hasa baada ya mpenzi wake wa zamani  Brown Mauzo kuanza mahusiano ya kimapenzi na  Vera Sidika

   Lakini  licha ya juhudi zake  kujaribu kuendelea na maisha yake bila kufuatiliwa  mama huyo wa mtoto mmoja amejipata tena  pabaya huku ikitolewa picha moja  inayomuonyesha akiwa ‘kwa mganga’ .

 Madai kama hayo sio mageni dhidi yake kwani wakati mmoja alidaiwa kujihusisha na mambo ya ushirikina wakati mke mwenza wake wa zamani    Aaliyah Zaheer,  alipoolewa na mfanyibiashara na mwanasiasa wa Kenya  Zaheer Jhanda.

 Mwanasosholaiti huyo  aliolewa kama mke wa pili wa mwanasiasa huyo wa Kisii  Zaheer kwa miaka mitatu  na wana mtoto wa kiume ,Gavin .

 Wakenya walimhoji kuhusu alichokuwa akifanya baada ya picha hiyo kumuonyesha akiwa amewashika kuku wawili na kufunikwa kitambaa .

 Lakini Amber alipata ujasiri wa kuyajibu maswali hayo  wakati shabiki mmoja alipotaka kujua mbona anatumia mambo ya ushirika .Faith alimuambia kwamba yeye katu hajawahi kushiriki mambo hayo

 Wengi hawakuridhika na jibu lake na akasema kwamba atapata muda baadaye kusema upand wake wa kisa  wakati mashabiki watakapokuwa tayari kumuamini .