logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Daktari bandia Mugo wa Wairimu ahukumiwa kifungo cha miaka 3 jela

Wairimu  pia alipatikana na hatia ya kuhudumu kama daktari bila leseni .mwaka wa 2018 Wairimu alikanusha mashtaka ya kuendesha kituo cha afya bila leseni na kuhudumu kama muuguzi bila leseni  kutoka kwa maamlaka husika

image
na Radio Jambo

Burudani28 October 2020 - 10:54

Muhtasari


  •  
  •  Mugo sio mgeni wa sakata kama hizo 
  • Ni mara ya pili anakabiliwa na mashtaka  hayo 

 

 

 Daktari bandia Mugo  Wa wairimu amepigwa faini ya shilingi milioni 1.4 na  endapo atakosa kulipa faini huyo atalazimika kuhudumia kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuendesha kituo cha afya bila leseni .

 Katika uamuzi wake uliotolewa siku ya jumatano hakimu mkuu mkaazi Martha  Nanzushi  amesema upande wa mashtaka umethibitisha kesi yake dhidi ya Mugo . pia alishtakiwa kwa kuendesha maabara bila  leseni kutoka kwa   baraza la wahudumu wa maabara nchini

Wairimu  pia alipatikana na hatia ya kuhudumu kama daktari bila leseni .mwaka wa 2018 Wairimu alikanusha mashtaka ya kuendesha kituo cha afya bila leseni na kuhudumu kama muuguzi bila leseni  kutoka kwa maamlaka husika .

 Muungano wa wauguzi ulijitenga naye ni mara ya pili kwake kutekeleza kosa hilo baada ya kuendesha klini yake mtaani Kayole .

  Katibu mkuu wa muungano wa kitaifa wa waugizi Seth panyako amesema Wairimu hayumo katika sajili ya wanachama wao .

Wairimu, alirejea katika vichwa vya habari  miaka michache baada ya kumdunga mwanamke mmoja dawa ya kulevya na kisha kumbaka  katika kliniki yake isiokuwa na kibali katika mta wa Githurai 44 akihudumu kama mwanajinakolojia

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved