logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IEBC: Kura ya maoni ya BBI kugharimu shilingi bilioni 14

Naibu afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo  Hussein Marjan amesema  tayari IEBC  imetengeza orodha ya mahitaji yake ili kufanikisha kura hiyo ya maoni .

image
na Radio Jambo

Habari28 October 2020 - 13:41

Muhtasari


 

  •  IEBC  imesema iko tayari kwa kura ya maoni 
  •  Tayari zimezuka pingamizi kuhusu mapendekezo ya BBI 

 

 

Kura  ya maoni kuhusu BBI itawagharimu wakenya shilingi bilioni 14

 Naibu afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo  Hussein Marjan amesema  tayari IEBC  imetengeza orodha ya mahitaji yake ili kufanikisha kura hiyo ya maoni .

" Tumeshaketi chini  na kujiuliza kuhusu yote tunayohitji .Itagharimu shilingi bilioni 14 kuandaa kura hiy’ amesema Marjan

 Amesema wamewazingatia wapiga kura milioni 19.6 na huenda idadi hiyo imeongezeka kwa sababu ya  kuendelea kwa mpango wa kuwasajili wapiga kura .

Marjan  ameyasema hayo alipofika mbele ya kamati ya  bunge kuhusu   uhasibu inayoongozwa na mbunge wa Ugunja Opiyo Wandayi

 Ripoti  ya BBI ilizinduliwa siku ya jumatatu huku mgawanyiko ukiibuka miongoni mwa viongozi wa kisiasa kuhusu baadhi ya mapendekezo yake . Naibu wa rais William Ruto amesimama kidete kupinga baadhi ya   mapendekezo hayo akisema yanafaa kujadiliwa kwa muda Zaidi lakini wanaunga mkono ripoti hiyo hawataki kutumiwa kwa muda Zaidi wa kuijadili au kuifanyia marekebisho wakati huu .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved