- IEBC imesema iko tayari kwa kura ya maoni
- Tayari zimezuka pingamizi kuhusu mapendekezo ya BBI
Kura ya maoni kuhusu BBI itawagharimu wakenya shilingi bilioni 14
Naibu afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo Hussein Marjan amesema tayari IEBC imetengeza orodha ya mahitaji yake ili kufanikisha kura hiyo ya maoni .
" Tumeshaketi chini na kujiuliza kuhusu yote tunayohitji .Itagharimu shilingi bilioni 14 kuandaa kura hiy’ amesema Marjan
Amesema wamewazingatia wapiga kura milioni 19.6 na huenda idadi hiyo imeongezeka kwa sababu ya kuendelea kwa mpango wa kuwasajili wapiga kura .
Marjan ameyasema hayo alipofika mbele ya kamati ya bunge kuhusu uhasibu inayoongozwa na mbunge wa Ugunja Opiyo Wandayi
Ripoti ya BBI ilizinduliwa siku ya jumatatu huku mgawanyiko ukiibuka miongoni mwa viongozi wa kisiasa kuhusu baadhi ya mapendekezo yake . Naibu wa rais William Ruto amesimama kidete kupinga baadhi ya mapendekezo hayo akisema yanafaa kujadiliwa kwa muda Zaidi lakini wanaunga mkono ripoti hiyo hawataki kutumiwa kwa muda Zaidi wa kuijadili au kuifanyia marekebisho wakati huu .