logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru aitisha mkutano huku visa vya Covid 19 vikiongezeka

Wakenya wengi wamerejelea shughuli za kawaida huku wakipuuza kanuni zote za kuzuia maambukizi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 October 2020 - 15:16

Muhtasari


 

  •  Serikali imehofishwa na ongezeko la visa vya maambukizi 
  • Wakenya wengi wamerejelea shughuli za kawaida huku wakipuuza kanuni zote za kuzuia maambukizi 

 

 

 Rais Uhuru Kenyatta ameitisha kikao kingine kuhusu corona  kati ya serikali kuu na zile za kaunti  kujadili ongezeko la visa vya maambukizi ya corona

 Kupitia taarifa  ta msemaji wa IKULU  Kanze Dena  ,mkutano huo utaandaliwa tarehe 4 mwezi Novemba .

" Kikao hicho  kimeitishwa kwa ajili ya kuongezeka kwa visa vya maambukizi ya corona  kote nchini  ikizingatiwa kwambakenya ilisajili idadi ya juu ya maafa mwezi oktoba mwaka huu kutokana na ugonjwa wa corona’ imesema taarifa hiyo

 Uhuru amewashauri wakenya kufuata kanuni zilizotolewa na serikali kupitia wizara ya afya ili kuzuia usambaaji wa virusi hivyo .

" wakenya wanafaa kuendelea kuvalia maski  kwa njia ifaayo wakiwa katika sehemu za umma  na kudumisha hali ya usafi wakato wote  kando na kuepuka maeneo yenye mrundiko wa watu’ taarifa hiyo imesema

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved