- Serikali imehofishwa na ongezeko la visa vya maambukizi
- Wakenya wengi wamerejelea shughuli za kawaida huku wakipuuza kanuni zote za kuzuia maambukizi
Rais Uhuru Kenyatta ameitisha kikao kingine kuhusu corona kati ya serikali kuu na zile za kaunti kujadili ongezeko la visa vya maambukizi ya corona
Kupitia taarifa ta msemaji wa IKULU Kanze Dena ,mkutano huo utaandaliwa tarehe 4 mwezi Novemba .
" Kikao hicho kimeitishwa kwa ajili ya kuongezeka kwa visa vya maambukizi ya corona kote nchini ikizingatiwa kwambakenya ilisajili idadi ya juu ya maafa mwezi oktoba mwaka huu kutokana na ugonjwa wa corona’ imesema taarifa hiyo
Uhuru amewashauri wakenya kufuata kanuni zilizotolewa na serikali kupitia wizara ya afya ili kuzuia usambaaji wa virusi hivyo .
" wakenya wanafaa kuendelea kuvalia maski kwa njia ifaayo wakiwa katika sehemu za umma na kudumisha hali ya usafi wakato wote kando na kuepuka maeneo yenye mrundiko wa watu’ taarifa hiyo imesema