logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Serikali kuunda hazina ya kuwasaidia wasio na ajira

Chelugui amesema hazina hiyo itawasaidia wasio na ajira na wanaopoteza kazi zao

image
na Radio Jambo

Habari20 November 2020 - 11:31

Muhtasari


 

  •  Chelugui amesema hazina hiyo itawasaidia wasio na ajira na wanaopoteza kazi zao 
  •  ILO imesema watu milioni 26 watakosa kazi kote duniani kwa ajili ya janga la corona 

 

 

Serikali ya kitaifa inapanga kuzindua hazina maalum ya kuwasaidia wafanyikazi wanaopoteza kazi zao .

Waziri wa Leba Simon Chelugui  amesema hazina hiyo itakuwa sehemu ya mpango wa kukwamua uchumi kutoka kwa makali ya janga la corona . Amesema licha ya mwongozo wa kupambana na corona kupunguza idadi ya maambukizi ,kanuni hizo pia zimesababisha watu wengi kupoteza kazi zao .

 Chelugui amesema serikali itafanya tathmini ya athari ya janga la corona kwa wafanyikazi wahamiaji .

 Biashara nyingi kote duniani na hasa zile ndogo ndogo na za kadri zimesajili hasara kubwa na nyingine kulazimika kufungwa .

 Sekta ya jua kali nchini Kenya amayo huwajiri asilimia 59.9 ya wafanyikazi imeshuhudia idadi kubwa ya watu waliopoteza kazi zao .

 Huduma za kijamii na kibinafasi kama vile saluni na  vinyozi pia zimeathiriwa – amesema Chelugui .

 Machi mwaka huu shirika la kimataifa la leba ILO lilisema kwamba janga la corona litasababisha  watu milioni 25 kote duniani kukosa ajira .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved