Hazina kuleta afueni

Serikali kuunda hazina ya kuwasaidia wasio na ajira

Watu wengi wamepoteza kazi zao

Muhtasari

 

  •  Chelugui amesema hazina hiyo itawasaidia wasio na ajira na wanaopoteza kazi zao 
  •  ILO imesema watu milioni 26 watakosa kazi kote duniani kwa ajili ya janga la corona 

 

 

Serikali ya kitaifa inapanga kuzindua hazina maalum ya kuwasaidia wafanyikazi wanaopoteza kazi zao .

Waziri wa Leba Simon Chelugui  amesema hazina hiyo itakuwa sehemu ya mpango wa kukwamua uchumi kutoka kwa makali ya janga la corona . Amesema licha ya mwongozo wa kupambana na corona kupunguza idadi ya maambukizi ,kanuni hizo pia zimesababisha watu wengi kupoteza kazi zao .

 Chelugui amesema serikali itafanya tathmini ya athari ya janga la corona kwa wafanyikazi wahamiaji .

 Biashara nyingi kote duniani na hasa zile ndogo ndogo na za kadri zimesajili hasara kubwa na nyingine kulazimika kufungwa .

 Sekta ya jua kali nchini Kenya amayo huwajiri asilimia 59.9 ya wafanyikazi imeshuhudia idadi kubwa ya watu waliopoteza kazi zao .

 Huduma za kijamii na kibinafasi kama vile saluni na  vinyozi pia zimeathiriwa – amesema Chelugui .

 Machi mwaka huu shirika la kimataifa la leba ILO lilisema kwamba janga la corona litasababisha  watu milioni 25 kote duniani kukosa ajira .