Muungano wa Milki za kiaranu UAE umefutilia mbali utoaji wa visa kwa wakenya wanaozuru taifa hilo na wageni kutoka nchi nyingine 11
Mataifa mengine yaliathiriwa na hatua hiyo ya UAE ni Pakistan, Iran, Yemen, Syria, Somalia, Iraq, Turkey, Afghanistan, Syria na Libya.
Hata hivyo ni Pakistan pekee iliyothibitisha habari hizo ikiwanukuu maafisa wa serikali .
Wizara ya mashauri ya kigeni ya Pakistan imesema marfuku hiyo haitawaathiri walio na visa tayari .
Haijabainika ni vitengo vipi vya visa ambavyo vimeathiriwa na hatua hiyo ya UAE .Kenya ilivunja rekodi ya maambukizi ya kila siku baaa ya visa Zaidi ya 1500 kuanza kuripotiwa huku idadi ya wanaofariki pia ikipanda .
Kwa sasa watu 1300 wamefariki kwa ajili ya ugonjwa huo huku Zaidi ya 70,500 wakiambukizwa .Mapema mwezi huu serikali ililazimika kupiga marufuku mikutano ya kisiasa ili kuzuia ongezeko la visa vya maambukizi