Uke wenza

DCI kumzuia seli mwanamke anayeshtumiwa kwa kumsakama hadi kufa mke mwenza

Mke wa kwanza anashtumiwa kwa kumuua wa pili

Muhtasari
  •  Mshukiwa alikuwa akiishi mashambani baada ya kutofautiana na mume wake 
  •  Alimwagia maji kabla ya kumsakama hadi kumwuua

 

Jescah Kalumu Mungatu

Makachero wa DCI siku ya ijumaa wameruhusiwa kumzuilia kwa siku 14 mwanamke anayeshtumiwa kwa kumuua mke mwenza kwa kumwagia maji na kisha kumnyonga hadi kumuua .

Jescah Kalumu Mungatu anashukiwa kumuua   kwa kumnyonga  Abbisseneh Katungu  baada ya kumwagia maji moto usiku ya tarehe 14 mwezi huu katika mtaa wa makadara ,Nairobi

 Kwa mujibu wa stakabadhi zilizowasilishwa kortini  kisa hicho kilitokea baada ya wanawake hao wawili kugombana wakati mume wao hakuwa nyumbani .

 Hakimu mkuu wa makadra  Heston Nyaga alikubali ombi la DCI kusalia na mshukiwa ili kuruhusu uchunguzi kuendelea

 DCI imesema tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi cha Lunga lunga na  mwenyekiti wa mta wa mabanda wa Sinai  Kioko Musau mwendo wa saa mbili usiku .

 Ripoti ya polisi imesema ,Mungatu ambaye ni mke wa kwanza  alikuwa akiishi mashambani baad ya kutofautiana na mume wake  .ni wakai alipokuwa  nyumani ndipo mume wake alimuoa Katungu kama mke wa pili . Baada ya mke wa kwanza kugundua kilichofanyika alifunga safari kuja Nairobi .

 Afisa nayechunguza kesi hiyo anasema  wanahitaji muda Zaidi  kumpeleska mshukiwa kwa ukaguzi wa akili . Amesema pindi uchunguzi utakapokamilishwa wataipeleka faili yake kwa DPP kwa maelekezo na ushauri .suala hilo litatajwa  Disemba tarehe 2