Corona

8 Wafariki huku 810 wakipatikana na Corona

Watu 265 wamepona ugonjwa huo

Muhtasari
  • Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema visa hivyo ni kutoka sampuli  7,387 zilizopimwa
  • Wagonjwa 31 wapo ICU .Watu 265 wamepona  ugonjwa huo na kufikisha 52,974 watu waliopona ugonjwa huo hadi kufikia sasa .
kagwe
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe kagwe

 Kenya siku ya jumatano imesajili visa vipya 810 vya corona  na kufikisha 79,322 jumla ya idadi ya visa hivyo nchini .

 Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema visa hivyo ni kutoka sampuli  7,387 zilizopimwa katika saa 24 zilziopita  na sasa idadi ya jumla ya  sampuli zilziopimwa ni 855,403 . idadi ya watu waliofariki kwa ajili ya Corona imeongezeka hadi  1,417  baada ya   watu  wanane  zaidi kuaga dunia .

Kagwe  amesema kwa sasa kuna wagonjwa 1,198 waliolazwa katika hospitali mbali mbali nchini huku watu 7,169 wakiwa chini ya mpango wa kutunzwa nyumbani .

 Wagonjwa 31 wapo ICU .Watu 265 wamepona  ugonjwa huo na kufikisha 52,974 watu waliopona ugonjwa huo hadi kufikia sasa .

 Katika visa vipya vilivyoripotiwa 792 ni wakenya ilhali 18 ni raia wa kigeni ,mgonjwa wa umri wa chini ana mwaka mmoja ilhali wa umri wa juu ana miaka 87 . watu 475 ni wanaume ilhali 335 ni wanawake