logo

NOW ON AIR

Listen in Live

8 Wafariki huku 810 wakipatikana na Corona

Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema visa hivyo ni kutoka sampuli  7,387 zilizopimwa

image
na Radio Jambo

Burudani25 November 2020 - 13:34

Muhtasari


  • Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema visa hivyo ni kutoka sampuli  7,387 zilizopimwa
  • Wagonjwa 31 wapo ICU .Watu 265 wamepona  ugonjwa huo na kufikisha 52,974 watu waliopona ugonjwa huo hadi kufikia sasa .
kagwe

 Kenya siku ya jumatano imesajili visa vipya 810 vya corona  na kufikisha 79,322 jumla ya idadi ya visa hivyo nchini .

 Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema visa hivyo ni kutoka sampuli  7,387 zilizopimwa katika saa 24 zilziopita  na sasa idadi ya jumla ya  sampuli zilziopimwa ni 855,403 . idadi ya watu waliofariki kwa ajili ya Corona imeongezeka hadi  1,417  baada ya   watu  wanane  zaidi kuaga dunia .

Kagwe  amesema kwa sasa kuna wagonjwa 1,198 waliolazwa katika hospitali mbali mbali nchini huku watu 7,169 wakiwa chini ya mpango wa kutunzwa nyumbani .

 Wagonjwa 31 wapo ICU .Watu 265 wamepona  ugonjwa huo na kufikisha 52,974 watu waliopona ugonjwa huo hadi kufikia sasa .

 Katika visa vipya vilivyoripotiwa 792 ni wakenya ilhali 18 ni raia wa kigeni ,mgonjwa wa umri wa chini ana mwaka mmoja ilhali wa umri wa juu ana miaka 87 . watu 475 ni wanaume ilhali 335 ni wanawake

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved