logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila: Mapendekezo ya BBI yanalenga kuboresha utawala wa Kenya

Odinga amesema masuala mengi yanaweza kushughulikiwa kupitia sheria na sera za serikali

image
na Radio Jambo

Burudani25 November 2020 - 10:16

Muhtasari


  •  Odinga amesema masuala mengi yanaweza kushughulikiwa kupitia sheria na sera za serikali 
  •  Odinga amewahimiza wakenya kujitokeza na kuweka saini zao ili kufanikisha kura ya maoni 

 

 Kiongozi wa ODM Raila  Odinga  amesema kwamba  wajibu wa mchakato wa BBI ni kuimarisha utawala wa Kenya .

Raila Odinga  amesema  masuala yanayohusu wananchi na hali ya uchumi yanaweza kushughulikiwa kupitia sheria na sera za serikali . Alikuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa  ukusanyaji wa sahihi za BBI katika ukumbi wa KICC .

 Kuhusu wadhifa ya msimamizi wa idara ya mahakama ambalo limekuwa donda sugu katika ripoti ya BBI   Raila amesema  jopo la uteuzi litampa rais majina ya watu watatu ambao yatatumwa bungeni kupigwa msasa na kisha moja kuteuliwa na rais .

" Hilo litavuruga vipi  uhuru wa  idara ya mahakama? Raila amesema

" Tumepitia mengi ya uhasama na  siku ngumu  na hata vipindi vya kubaguliwa na tunaweza kuona tunakotaka kwenda’

 Amewahimiza wakenya kujitokeza kwa wingi na kutia saini  zinazohitajika kufanikisha kura ya maoni ili kuirekebisha katiba .

  


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved