- Odinga amesema masuala mengi yanaweza kushughulikiwa kupitia sheria na sera za serikali
- Odinga amewahimiza wakenya kujitokeza na kuweka saini zao ili kufanikisha kura ya maoni
Kiongozi wa ODM Raila Odinga amesema kwamba wajibu wa mchakato wa BBI ni kuimarisha utawala wa Kenya .
Raila Odinga amesema masuala yanayohusu wananchi na hali ya uchumi yanaweza kushughulikiwa kupitia sheria na sera za serikali . Alikuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa ukusanyaji wa sahihi za BBI katika ukumbi wa KICC .
Kuhusu wadhifa ya msimamizi wa idara ya mahakama ambalo limekuwa donda sugu katika ripoti ya BBI Raila amesema jopo la uteuzi litampa rais majina ya watu watatu ambao yatatumwa bungeni kupigwa msasa na kisha moja kuteuliwa na rais .
" Hilo litavuruga vipi uhuru wa idara ya mahakama? Raila amesema
" Tumepitia mengi ya uhasama na siku ngumu na hata vipindi vya kubaguliwa na tunaweza kuona tunakotaka kwenda’
Amewahimiza wakenya kujitokeza kwa wingi na kutia saini zinazohitajika kufanikisha kura ya maoni ili kuirekebisha katiba .