logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru:Heri nilale kuliko kuingia Twitter

Rais amesema anapendelea kukutana ana kwa ana na viongozi kwa majadiliano badala ya kutegemea twitter

image
na Radio Jambo

Habari25 November 2020 - 11:14

Muhtasari


 

  •  Rais amesema anapendelea kukutana ana kwa ana na viongozi kwa majadiliano badala ya kutegemea twitter 
  •  Rais kenyatta alikuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi la kukusanya sahihi za BBI 

 

 

 Rais Uhuru kenyatta alizua  kicheko siku ya jumatano aliposema mbona hataki kuingia twitter na  mitandao ya kijamii . Rais ambaye alikuwa akieleza kuhusu mikutano ambayo  amekuwa akifanya na viongozi   mbali mbali ili kusikiliza kuhusu mapendekezo yao  kuhusu BBI rais alisema  hategemi Twitter kupata maelezo na mapendekezo ya  wengine . Rais  amesema ;

 ‘Mimi sipendi kwa magazeti ,mimi nakutana na watu tu ….kwa sababu mimi sio mtu  wa hiyo . Hata twitter niliondoka …hii kitu ni bure…! ni matusi tu .. hakuna kitu inaendelea .unakaa hapo unasoma hulali ….unasomaaa …huyu ..unapiga simu unaona vile huyu mtu amenitusi ..afadhali nilalale bwana .. niongee…nipige story na mama hapo  kidogo hapo ..nilale niamke ..niende kazi ..dunia iendelee …’

 Kumekuwa na ongezeko la matumizi ya mitandao  ya kijamii na hasa twitter kueleza misimamo mbali mbali ya kisiasa huku naibu rais William Ruto akiwa miongoni mwa viongozi wanaotumia sana twitter .

 Ruto amekuwa akitumia sana twitter kupaza sauti yake kuhusu masuala mbali mbali lakini yaonekana mkuu wake hapendi mbinu hiyo ya mawasiliano .

Rais alikuwa akizungumza siku ya jumatano wakati wa uzinduzi wa  ukusanyaji wa sahihi za kufanikisha kura ya maoni kupitia BBI . Amesema  mapendekezo ambayo yametolewa na wakenya mbali mbali yatazingatiwa lakini wananchi wanafaa kufahamu kwamba katiba inaweza kurekebishwa kwa awamu kulingana na mahitaji ya wakati uliopo

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved