- Barasa amesema ataongoza kampeini za kupinga BBI
- Mbunge huyo ameongeza kwamba maoni katika BBI sio ya wakenya wote bali ya wachache
Mbunge wa kimilili Didmus Barasa amesema yuko tayari kuongoza kampeini ya kupinga BBI akiongeza kwamba mapendekezo katika ripoti hiyo hayasaidia kushughulikia matatizo yanayowakumba wakenya .
Barasa, ambaye ni mshirika wa karibu wa naibu wa rais William Ruto ames ema ripoti ya BBI haiwakilishi maoni ya wakenya wengi kwani haishughulikii masuala kama vile ya ukulima na kuwalinda wafanyibiashara wadogo wadogo .
" Wakenya wamedanganywa kuamini kwamba unaweza tu kufaulu iwapo mtu wa jamii yako yupo katika nafasi ya juu ya uongozi .Ndio kwa sababu BBI inaongeza nafasi katika serikali na kuzidisha idadi ya wabunge’ amesema Barasa .
" Maoni ya wakenya wote ni muhimu . maoni ya watu waliovalia suti za bei ya juu sio muhimu kuliko za mama mboga ‘ amesema
Barasa amesema hataraji kujipata pabaya machoni mwa serikali anapoanza kampeini ya kuwashawishi wakenya kuikataa ripoti ya BBI kupitia kura ya maoni kwa sababu Kenya ni nchi ya Kidemokarsia