logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tuko tayari kupigana na vyama vingine katika kinyanganyiro cha Urais' Chama cha NRA chaapa

Chama hicho ambacho kitazinduliwa rasmi mwezi Machi ama April kwa sababu ya corona,

image
na Radio Jambo

Habari20 January 2021 - 09:47

Muhtasari


  • Chama cha NRA chaapa kupigana na vyama vingine vya kisiasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022

Chama kipya cha kisiasa cha National Reconstruction Alliance kimeahidi kuonyesha vyama vingine kivumbi mwaka wa 2022.

Chama hicho kilichosajiliwa hivi majuzi na Wakili Riziki Dunstan na wenzake Amemba Magufuli na Fred Ojiambo tayari kina memba 500,000.

Chama hicho ambacho kitazinduliwa rasmi mwezi Machi ama April kwa sababu ya corona, kimewaomba vijana kujiandaa kupiga kura mwaka wa 2022.

 

Katika ujumbe wake kwa wanahabari msimamizi wa vijana Kisii Joshua Nyabanayo ameomba vijana kujitayarisha kwa shughuli hii kwa kuchukua vitambulisho na kadi za kupiga kura.

Vile vile Lumala Lumala ambaye ni msimamizi wa wanafunzi katika chuo kikuu cha Masinde Muliro amesemaViongozi wa vyama vikongwe watakiona Cha mtema kuni mwaka wa 2022.

"Kama chama tuko tayari kupigana na vyama vikuu hapa Kenya.Wanafaa wawe tayari kupigana Vita,ngumu zaidi maishani mwao."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved